Mwalimu ajiua kwa kujichinja koromeo...Soma habari kamili na Matukio360..#share

Na Mwandishi Wetu

Leonard Mwipugi (29) ambaye ni Mwalimu wa Shule ya Sekondari ya Mtenga wilayani Nkasi, amejiua kwa kujichinja koromeo akiwa nyumbani kwake.

Akithibitisha kutokea kwa tukio Mratibu wa Elimu Kata ya Mtenga, Hebron Mwafungo amebainisha kwamba Mwipugi amekutwa akiwa amekufa baada ya kujichinja.

Amefafanua kuwa marehemu amafanya kitendo hicho nyumbani kwake jana  saa sita mchana.

Aidha Mwafungo amesema kabla ya mwalimu huyo kukutwa amejiua, alikwenda kazini kwake na saa 5 alirejea nyumbani ambapo hakumkuta mkewe.

Ameelza  baada ya muda walipata taarifa kuwa mwalimu huyo amekutwa amekufa baada ya kujichinja koromeo akiwa chumbani kwake.

Amebainisha kwamba licha Mwipugi kuishi na mkewe alikuwa pia akiishi na mdogo wake na wakati wa tukio hilo alikuwa  amemtuma mbali kidogo ya nyumbani.


Hivyo baada ya mdogo huyo kurudi aliona damu zikichuruzika na alipochungulia chumbani alikuta kaka yake amekwishafariki.

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search