Naibu Waziri Mabula atoa siku 90 kwa Ofisa Ardhi Hanang...Soma habari kamili na Matukio360..#share


NAIBU Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dk. Angeline Mabulla ametoa siku 90 kwa Ofisa Ardhi Mteule wa Halmashauri ya wilaya ya Hannang mkoani Manyara, Egidius Kashaga kurekebisha mfumo wa uhifadhi wa hati za umiliki ardhi.
Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dk. Angeline Mabulla akipekua mafaili ya kuhifadhia hatimiliki za ardhi wakati alipofanya ziara ya kushtukiza katika idara ya ardhi ya halmashauri ya wilaya ya Hannang na kukuta mfumo mbovu wa uhifadhi wa hati za kumiliki ardhi hali ambayo ni rahisi kwa maafisa hao kudanganya na kumilikisha mtu zaidi ya mmoja.

Imebainika kuwa mifumo hiyo inamapungufu ambayo ni rahisi kwa maofisa hao kudanganya na kumilikisha ardhi kwa watu zaidi ya mmoja.

Mabula ameyasema hayo leo wakati alipofanya ziara ya kushtukiza katika idara ya ardhi ya halmashauri ya wilaya hiyo.

“Nakupa siku 90 uwe umerekebisha huu mfumo, na kama ndani ya kipindi hiki utashindwa kutekeleza agizo hilo nitakuvua cheo chako na kukuadhibu kwa mujibu wa sharia,” amesema Mabula.

Wakati wa ziara hiyo Mabulla ameamua kupekua Hati za mwananchi mmojammoja na kugundua baadhi ya hati hizo hazina vielelezo vya kumbukumbu na baadhi ya nyaraka za umiliki wa ardhi hazina mtiririko mzuri wa uhifadhi wa mafaili.

Katika hatua nyingine Mabulla amekutana na wananchi wa Kata ya Mogitu, Wilaya humo na kusikiliza kero zao za ardhi hasa suala la muwekezaji wa Kiwanda cha Manyara Cement Limited ambaye ameomba eneo la ujenzi wa kiwanda la ukubwa wa ekari 370.

Mmiliki huyo James Mtei alipeleka maombi yake kwa Halmashauri ya Wilaya ya Hannang akiomba ardhi katika kijiji cha Mogitu ili ihawilishwe na imilikishwe kwa Kampuni yake kwa hati miliki chini ya Sheria ya Ardhi (Sura 113) kwa ajili ya ujenzi wa kiwanda cha uzalishaji saruji.

Kwa mujibu wa Sheria hiyo ili mtu au kampuni iweze kumilikishwa ni lazima maombi hayo yaridhiwe na wanakijiji na kumfikia Waziri wa Ardhi na baadae kuidhinishwa na Mheshimiwa Raisi ikiwa ataridhia kutoa kibali chake cha Uhawilishaji.


Mabulla ametembelea eneo hilo linalotaraji kujengwa Kiwanda cha uzalishaji saruji ili aweze kujiridhisha kabla ya kummilikisha mwekezaji huyo.

Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mheshimiwa Dk. Angeline Mabulla akiongea na wananchi wa Kata ya Mogitu, Wilaya ya Hanang mkoani Manyara mara baada ya kusikiliza kero zao za ardhi hasa suala la muwekezaji wa Kiwanda cha Manyara Cement Limited ambacho kimeomba eneo la ujenzi wa kiwanda la ukubwa wa ekari 370.

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search