Watanzania watahadharishwa kuhusu Bangi...soma habari kamili na Matukio360...#share
Mkuu wa wilaya hiyo Rehema Madusa ameimbia Matukio360 kuwepo
kwa taarifa za watu wachache
kuendeleza kilimo cha
bangi katika baadhi ya mashamba na misitu iliyopo wilayani humo.
“Kata ya Matwiga ni
mojawapo ya maeneo ambayo kilimo cha bangi kinaendelea, hii inatokana na baadhi
ya viongozi kuwaficha kwa maslahi yao,” amesema
Amesema pamoja na
changamoto hiyo atashirikiana na wananchi waadilifu kuwabaini wanaondeleza
kilimo hicho
"Wananchi ndio
wanaotambua mienendo ya wakulima na wale wanaolima bangi, sasa watoe ushirikiano kwa Serikali. Bangi ni mojawapo ya
madawa ya kulevya
hivyo hatuwezi kukubali vizazi viharibike.”
Pamoja na mambo
mengine Madusa ameiagiza kamati ya ulinzi
na usalama wilaya humo kufanya uchunguzi wa kina kuhusu suala hilo.
Ofisa Mtendaji kata
ya Matwiga, Moses Rudisha amethibitisha kuwapo kwa hali hiyo na kwamba
changamoto ni namna ya kuwafikia
kutokana na umbali wa maeneo inapolimwa bangi.
"Katika kata hii bangi inalimwa kwa
vificho na kwenye mapoli pia miundombinu ya huku si salama na rafiki."amesema.




No comments:
Post a Comment