RC Rukwa asifu juhudi zinazofanywa na TAWA
Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Steve Zelote (Kamishna mstaafu wa Jeshi la Polisi) amekutana na uongozi wa Mamlaka ya Usimamizi Wanyamapori Tanzania - TAWA ofisini kwake Mjini Sumbawanga.
Akiongoza mkutano huo, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa TAWA Dkt. Wakibara amewataka watumishi wa pori la Lwafi kufanya kazi kwa bidii na kutojiusisha na vitendo vya rushwa.
Nae Mkuu wa Mkoa amesifu juhudi zinazofanywa na askari wanyamapori kutoka mapori ya Akiba Uwanda na Lwafi Mkoani Rukwa, hasa suala la kuondoa ng'ombe Ndani Ya hifadhi.
Aidha, Mkuu wa Mkoa amemuomba Dkt. Wakibara kusaidia operesheni za kuondoa mifugo katika wilaya zote za Mkoa wake.
Kaimu Mkurugenzi Mkuu. TAWA yuko katika ziara yake ya kutembelea Mapori Akiba(Game Reserves). Baada ya safari yake ya kutoka Mkoa wa Katavi na Rukwa ataendelea Mkoa wa Singida na Mbeya kutembelea Pori la Rungwa/Kizigo/Muhesi liliopo katika mikoa hii miwili ili aweze kuongea na watumishi wa mapori hayo na kusikiliza changamoto mbalimbali za utendaji kazi na kujadiliana nao kuona uwezekano wa kuzitatua
Taarifa hii imeandikwa na Bw. Twaha Twaibu (Afisa habari na Mahusiano -TAWA)
Akiongoza mkutano huo, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa TAWA Dkt. Wakibara amewataka watumishi wa pori la Lwafi kufanya kazi kwa bidii na kutojiusisha na vitendo vya rushwa.
Nae Mkuu wa Mkoa amesifu juhudi zinazofanywa na askari wanyamapori kutoka mapori ya Akiba Uwanda na Lwafi Mkoani Rukwa, hasa suala la kuondoa ng'ombe Ndani Ya hifadhi.
Aidha, Mkuu wa Mkoa amemuomba Dkt. Wakibara kusaidia operesheni za kuondoa mifugo katika wilaya zote za Mkoa wake.
Kaimu Mkurugenzi Mkuu. TAWA yuko katika ziara yake ya kutembelea Mapori Akiba(Game Reserves). Baada ya safari yake ya kutoka Mkoa wa Katavi na Rukwa ataendelea Mkoa wa Singida na Mbeya kutembelea Pori la Rungwa/Kizigo/Muhesi liliopo katika mikoa hii miwili ili aweze kuongea na watumishi wa mapori hayo na kusikiliza changamoto mbalimbali za utendaji kazi na kujadiliana nao kuona uwezekano wa kuzitatua
Picha ya pamoja Mkuu wa Mkoa(wa nnne kutoka kushoto) na Kaimu Mkurugenzi Mkuu TAWA (wa tano kutoka kushoto) pamoja na maafisa wa TAWA na ofisi ya RC mbele ya jengo la Mkuu wa Mkoa |
Picha ya pamoja Kati ya Kaimu Mkurugenzi Mkuu-TAWA(wa tano kutoka kulia) na askari wa Pori la akiba la Lwafi |
Mbao zaidi 200 zilizokamatwa zimevunwa na majangili Ndani ya pori la Lwafi |
Baadhi ya askari wa pori la akiba Lwafi wakimsililiza kwa makini Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa TAWA (haonekani kwenye picha) |
Bw. Pascal Mrina aliyesimama, (Meneja. wa Mapori ya Akiba Uwanda na Rukwa-Lwafi) |
Dkt. Wakibara akisisitiza Jambo alipokuwa akiongea na watumishi wa pori la akiba Lwafi(hawaonekani kwenye picha hii) |
Askari wa pori la Akiba Uwanda |
Jengo la Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Rukwa |
Ng'ombe 319 wamekamatwa Ndani. Ya pori la Akiba Uwanda |
Taarifa hii imeandikwa na Bw. Twaha Twaibu (Afisa habari na Mahusiano -TAWA)
No comments:
Post a Comment