TWAWEZA: Asilimia 67 wanataka katiba mpya...soma habari kamili na Matukio360..#share

Na Abraham Ntambara
TAASISI isiyokuwa ya kiserikali ya TWAWEZA imesema asilimia 65 ya watanzania wanataka katiba mpya.


Mkurugenzi Mtendaji wa Twaweza Aidan Eyakuze akizungumza wakati wa uzinduzi wa matokeo ya utafiti waliofanya juu ya Katiba Mpya jijini Dar es Salaam

Wakati utafiti huo wa Twaweza ukionyesha wananchi wengi wakidai Katiba Mpya  Rais John Magufuli amesema kwa sasa Katiba mpya sio kipaumbele cha serikali yake .

Twaweza inayohusika na masuala ya utafiti nchini inaeleza kuwa asilimia 67 ya wananchi nchini wanataka  katiba mpya.

Mkurugenzi Mtendaji wa taasisi hiyo Aidan Eyakuze amesema utafiti  wao uliitwa   ‘Zege imelala?’ Maoni ya wananchi kuhusu kukwama kwa mchakato wa kuunda katiba mpya.

Amesema utafiti huo unatokana na takwimu za sauti ya wananchi, utafiti wa kwanza barani Afrika wenye uwakilishi wa kitaifa unaotumia simu za wananchi ambapo amefafanua matokeo hayo yanatokana na takwimu zilizokusanywa kutoka kwa wahojiwa 1,745 kutoka maeneo mbalimbali ya Tanzania Bara mwezi Juni hadi Julai mwaka huu.

“ Wananchi wanataka Katiba mpya. Wengi wao wanataka mchakato uanze upya na tume mpya katika ukurasa mpya. Hata hivyo, wapo wananchi amabo wapo tayari kusonga mbele kwa kutumia rasimu iliyoandaliwa na tume iliyotangulia,” amesema Eyakuze.

Aidha katika utafiti huo Eyakuze amesema asilimia 56 wametaka toleo la mwisho la rasimu ya katiba lipigiwe kura na wananchi huku asilimia ya 48 ya wananchi wakabainisha kuwa Katiba mpya haitapatikana ndani ya miaka mitatu ijayo.
Amebainisha, wananchi wameendelea kuunga mkono kwa nguvu uundwaji wa katiba mpya inayotilia mkazo suala la uwajibikaji ambapo asilimia 79 wanataka mawaziri wawe na uwezo wa kuwaondoa wabunge katikati ya chaguzi iwapo hawatatekeleza majukumu yao ipasavyo.

Hata hivyo Eyakuze ameeleza kwamba wananchi wamegawanyika kwenye baadhi ya hatua katika uwajibikaji zilizopendekezwa ikiwemo kuzuia viongozi na watumishi wa umma kuwa na akaunti nje ya nchi ambapo asilimia 52 wanaunga mkono kuwepo kwa ukomo wa ubunge , asilimia 52 wanaunga mkono na kuweka kanuni za uwazi na uwajibikaji kuwa sehemu ya tunu ya Taifa.

Aidha wananchi wanaunga Mkono kuondolewa kwa kipengele kinachotaka kuchunguza na kudhibiti Ofisi ya Rais ambao ni asilimia 56 pamoja na mawaziri kuchaguliwa nje ya bunge asilimia 62.

Akizungumzia muundo wa serikali unaotakiwa katika katiba hiyo mpya Eyakuze amesema asilimia 42 ya wananchi waliunga mkono muundo wa serikali mbili huku muundo wa serikali moja ukiungwa mkono kwa asilimia 25 wakati wa serikali tatu ukiwa kwa asilimia 16.

Katibu wa Itikadi na Uenezi wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Humphrey Polepole akichangia maoni yake juu ya utafiti huo, amesema hana shaka na utafiti huo, lakini amesisitiza kuwa pamoja na kutakiwa kwa katiba mpya cha muhimu ni viongozi waliopewa dhamani kuiishi katika katika kuwatumikia wananchi.

Naye Mwanaharakati wa Haki za Binadamu Deogratius Bwire amesema kuwa cha muhimu ni kuwa na Katiba mpya iliyoandikwa ili mwananchi awe na haki ya kudai kitu ambacho kimo ndani ya katiba kwani Katiba ndiyo mfumo mzima wa mwongozo wan chi.



Mwanaharakati wa Haki za Binadamu Daogratius Bwire akitoa maoni yake juu ya Utafi wa Twaweza Juu ya Katiba Mpya  jijini Dar es Salaam.

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search