Waziri Kalemani azibana kampuni za mafuta..soma habari na Matukio360...#share
Salha Mohamed
Meneja bohari kutoka kampuni ya puma, Auni Yeteri akimuonesha Waziri wa Nishati, Dk. Medard Kalemani matanki ya kuhifadhia mafuta alipofanya ziara katika kampuni hiyo Kurasini jijini Dar es Salaam Leo
SERIKALI
imezitaka kampuni za kuhifadhi mafuta (Tiper) na Puma kutoa taarifa za shughuli
wanazofanya kila baada ya miezi mitatu.
Hatua hiyo imefikiwa kutokana na kampuni hizo kutotoa taarifa za shughuli zao ikiwamo mapato serikalini.
Hatua hiyo imefikiwa kutokana na kampuni hizo kutotoa taarifa za shughuli zao ikiwamo mapato serikalini.
Agizo hilo
limetolewa leo jijini Dar es Salaam na Waziri wa Nishati
Dk Medard Kalemani na kwamba serikali inaziangalia kampuni hizo kwa macho
ya ndani na kuangalia shughuli wanazozifanya za kiutendaji kila baada ya miezi
mitatu.
“Katika
makampuni haya Serikali ina hisa ya asilimia 50 kupitia msajili wa hazina na hazijawahi kutoa taarifa ya shughuli zao
serikalini.” Amesema na kuongeza “Hivyo kila baada ya miezi mitatu mnatakiwa
kuleta ripoti zenu serikalini ikiwamo za mapato.”
Amesema kutaka
taarifa hizo ni serikali kutaka kujua kinachoendelea na kinyume na hapo
watachukuliwa hatua kali za kisheria.
Pia ameyataka makampuni hayo kumaliza ukarabati
wa matenki ya kuhifadhia mafuta ndani ya wiki moja.
"Kampuni
ya Puma haijafika mikoa sita nchini, sasa
mfungue vituo mikoa yote hadi kufika mwakani ili msilalamikie mapato mkifika
mikoa yote itasaidia kuongeza mapato kwa sababu mahitaji yapo...ikifika Januari
mwakani nitafuatilia."amesema
Amesema kwa
sasa Wizara yake imeweka dawati maalumu la kufuatilia Puma hivyo wajitahidi
kutatua changamoto za kampuni hiyo na kuwataka wafanyakazi kuwa wazalendo na
kuacha kushirikiana na walinzi kuiba mafuta.
Baadhi ya
wafanyakazi wa Kampuni ya Puma, wamesema kumekuwa na changamoto ya meli
kushusha mafuta kwa siku 10 badala ya siku 5 jambo linalosababisha wakati
mwingine vituo kukosa mafuta.
Kwa upande
wake Msaidizi wa Mkurugenzi Kampuni ya Tiper, Paulo Mzava amesema kampuni hiyo
imechangia asilimia 68.5 ya mapato serikalini huku ikiwa imeagiza Flow mita
sita ili kuongeza mapato zaidi
No comments:
Post a Comment