'Updates' kutoka anapohojiwa Zitto Kabwe atuhumiwa kwa makosa mawili...soma habari kamili na Matukio360..#share
Na mwandishi wetu
KIONGOZI wa Chama cha ACT Wazalendo, Zitto Kabwe, anaendelea kuhojiwa na Polisi katika kituo kikuu cha Chang'ombe wilayani Temeke jijini dar es salaam akituhumiwa kufanya makosa mawili ya uchochezi.
Zitto Kabwe
Afisa
Habari wa ACT Wazalendo, Abdallah Khamis ameiambia Matukio360 kuwa katika
mahojiano hayo, Zitto ameambata na timu
ya wanasheria wa chama hicho akiwamo wakili Steven Mwakibola na Venas Msebo.
Miongoni
mwa makosa anayoojiwa ni kwamba Jumapili ya Oktoba 29, 2017 alipokuwa kwenye mkutano wa
kuzindua kampeni za udiwani katika Kata ya Kijichi, Wilayani Temeke alitoa
maneno yanayoweza kupelekea uvunjifu wa amani. Maneno hayo ni yafuatayo:
1.
Kwamba wananchi wasiichague CCM kwa sababu Serikali yake imeshindwa kufanya
uchunguzi na kuwakamata watu waliompiga risasi Mbunge Tundu Lissu mpaka siku
hiyo.
2.
Kwamba wananchi wasiichague CCM kwa sababu Serikali yake imeshindwa kueleza
chanzo cha miili ya watu wanaookotwa kwenye fukwe za bahari kama Coco Beach.
Hivyo kuichagua CCM ni sawa na kuwaunga mkono waliofanya vitendo vya
kumshambulia Tundu Lissu na wanaoua watu wanaookotwa kwenye fukwe.
No comments:
Post a Comment