Waziri Lukuvi awapa mtihani Wakurugenzi, Maafisa Ardhi, Ujenzi na Mipango miji..Soma habari kamili na Matukio360..#share
WAZIRI wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi William Lukuvi
amewaagiza Wakurugenzi wa Halmashauri, Maafisa Ardhi, Maafisa Ujenzi na Maafisa
Mipangomiji kuweka alama za X na kuvunja majengo yote yanayojengwa katika miji
yao bila kibali.
WAZIRI wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi William Lukuvi (katikati) akisoma nyaraka.
Aidha ameagiza pia kuvunjwa majengo yaliyojengwa katika
viwanja vya watu wengine kwa kumiliki
hati za ardhi kwa dhuruma.
Ametaka shamba hilo lirejeshwe serikalini kwa kuwa utaratibu wa kuligawa
umekiukwa kwa kiwango kikubwa huku masharti ya uendeshaji yakiwa hayajazingatiwa.
Amesema tatizo la ujenzi holela huchangiwa na Wakurugenzi wa
Halmashauri, Maafisa Ardhi, Maafisa Ujenzi na Maafisa Mipango miji ambao
wanaacha majengo yanajengwa katika miji yao bila kujua ujenzi huo umefuata
taratibu.
Lukuvi amesema atapambana na viongozi hao pale ambapo atakuta
majengo yamekithiri katika miji yao na hayana vibali vya ujenzi.
Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Kamishna Mstaafu Zelote Stephen
amemhakikishia Waziri Lukuvi kuwa atayafanyia kazi mapendekezo yake kikamilifu
na kwa haraka ili kuondoa migogoro na kero zinazoukabili mkoa wake katika
masuala yote ya ardhi.
No comments:
Post a Comment