Waziri Mwakyembe mgeni rasmi mkutano viongozi wa Dini...Soma habari kamili na Matukio360


Na Abraham Ntambara

WAZIRI wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Dk. Harrison Mwakyembe anatarajiwa kuwa mgeni rasmi katika mkutano wa viongozi dini wenye lengo la kubadilishana mawazo kuhusu  masuala ya kiimani, kijamii  na kiuchumi.

Mkurugenzi wa Msaidizi Lugha kutoka Wizara ya Habari Utamaduni Sanaa na Michezo, Hajjat Shani Kitogo (katikati) akizungumza na waandishi wa habari  kuhusu mkutano wa viongozi wa madhehebu ya dini uliyoandaliwa na Wizara ya Habari Utamaduni Sanaa na leo jijini Dar es Salaam.

Hayo yamebainishwa leo jijini Dar es Salaam na Mkurugenzi Msaidizi Lugha kutoka Wizara ya Habari Utamaduni Sanaa na Michezo, Hajjat Kitogo alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari kuhusu maandalizi ya mkutano huo ambao utafanyika Oktoba 25/2017 .

“Sera ya Utamaduni ya Mwaka 1999 Sura ya Nane inazungumzia Malezi na inasema mafunzo ya dini yatakuwa sehemu ya malezi ya watoto ili kusisitiza Maadili,Malezi Mema,Kazi, Kustahiana na Kuvumiliana, alisema Hajjat Kitogo.
Aidha amesema serikali inatambua umuhimu wa Viongozi wa Dini katika ulezi wa jamii na maendeleo ya Taifa na ndiyo maana imeona ni vyema kukutana nao na kujadili  namna gani itaweza kulisimamia taifa katika kufikia malengo.
Naye mmoja wa washiriki wa mkutano huo  Hadija Kisubi ametoa maoni yake na kusema anaamini viongozi wa dini wanamchango mkubwa katika kujenga nidhamu ya kwa taifa sababu ya neema ya mungu iliyondani ya viongozi hao pale wanatoa maelekezo kwa umma.
Pamoja na hayo mkutano huo umebeba Kauli Mbiu inayosema “Imani na Uzalendo Kuelekea Uchumi wa Viwanda,” amesema.

                        **************************MWISHO************************




















































About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search