Ajali 1375 zatokea Julai hadi Septemba...soma habari kamili na Matukio360..#share
Salha
Mohamed
JESHI
la Polisi kikosi cha usalama barabarani limesema ajali za barabarani zimepungua
kwa asilimia 48 ukilinganisha na mwaka 2016 na ajali 1375 zimetokea kati ya
Julai na Septemba 2017.
Kamanda wa polisi kikosi cha Usalama barabarani, Fortunatus Musilimu akizungumza na waandishi wa habari katika uzinduzi wa wiki ya nenda kwa usalama mkoani Dar es Salaam, maadhimisho hayo yanatarajia kufanyika katika viwanja vya biafra kuanzia Novemba 18 hadi 25, 2017.
Kamanda
wa Polisi kikosi cha Usalama barabarani, Fortunatus Musilimu amesema hayo jijini Dar es Salaam kwenye uzinduzi wa wiki ya nenda kwa usalama itakayoanza
Novemba 18 hadi 25, 2017 katika viwanja va Biafra na kuwa takwimu hizo ni za
nchi nzima.
Amesema
ajali hizo zimesababisha vifo vya watu 625, majeruhi 1486 ukilinganisha na
mwaka 2016 katika kipindi kama hicho kulikuwa na ajali 2639, vifo 923 na
majeruhi 2460 ambapo takwimu zinaonesha
upungufu wa ajali ni 1264 sawa na asilimia 48, upungufu wa vifo 298 sawa na
asilimia 32 huku pungufu ya majeruhi ikiwa 974 sawa na asilimia 40.
“Kabla ya kuanza maadhimisho ya wiki ya nenda
kwa usalama barabarani mkoani Kilimanjaro kuanzia Oktoba 9 hadi 15, 2017
kulikuwa na ajali 46, vifo 56 na majeruhi 35 …wiki ya maadhimisho ya usalama wa
barabarani kuanzia Oktoba 16 hdi 22 mwaka huu kulitokea ajali 37 vifo 48 na
majareruhi 32,”amesema.
Amesema
kutokana na takwimu hizo na kutoa elimu ya usalama barabarani wamepunguza ajali
9 sawa na asilimia 20, vifo 8 sawa na asilimia 14 na majeruhi 3 sawa na
asilimia 7 na kuwa maadhimisho hayo yamesaidia.
Amesema
takwimu za maadhimisho yaliyofanyika Septemba 26, hadi Oktoba 2,2016 kulitokea ajali 50, vifo 49 na majeruhi 42
ukilinganisha na maadhimisho yaliyofanyika mkoani Kilimanjaro kuanzia Oktoba 16
hadi 22, 2017 kulikuwa na ajali 37 vifo 48 na majeruhi 32.
Ameishukuru
benki ya stanbic kwa kutambua juhudi ambazo wanazifanya katika kukabiliana na
ajali za barabarani nakuhakikisha elimu inatolewa kwa watu wengi na kwa muda
mfupi ili kusasaidia kuokoa maisha ya watanzania.
Amewataka madereva kutii
sheria bila shuruti na watachukulia hatua kali za kisheria madereva wazembe
Kwa
upande wake mkuu wa matawi na mitandao wa Benki ya Stanbic, Musa Kitoa amesema lengo
lao ni ifikapo mwaka 2020 ajali zipungue hadi asilimia 50.
“Tutatoa
elimu kwa watu wengi, tutatengeneza video, stika atakayeona usalama barabarani
si mzuri apige simu kuwajulisha wahusika, tumeandaa watu kwa ajili ya kutoa
alimu kwa madereva wa magari yanayobeba wanafunzi,”amesema.
No comments:
Post a Comment