Askofu ampa 'tano' Magufuli...soma habari kamili na Matukio360..#share

Salha Mohamed
MWENYEKITI wa taasisi ya Good News for All Ministry, Askofu Dk Charles Gadi amempongeza rais  Dk John Magufuli kwa kusimamia rasilimali za nchi na kurejesha malimbikizo ya kodi.

Mwenyekiti wa taasis ya Good News For All Ministry Dk. Charles Gadi (katikati) akiendesha maombi ya kuomba mvua isilete madhara kwa jamii leo jijini Dar es Salaam, kushoto ni Mchungaji James Mwageni, kulia ni Mchungaji Palemo Massawe.

Pongezi hizo amezitoa leo jijini Dar es Salaam alipozungumza na waandishi wa habari lengo likiwa ni kuomba mvua zinazonyesha zisilete maafa kwa wananchi na kumpongeza rais kwa juhudi za kusimamia ipasavyo rasilimali za nchi.

Amesema rais amefanikiwa kusimamia eneo la madini ya dhahabu na vito kwa kiwango cha kuwezeshwa kurudisha sehemu ya malimbikizo ya kodi ambayo kwa namna moja au nyingine huenda zisingerudishwa.

“….tusingezipata kama si msimamo wake wa kutoyumba dhidi ya makampuni ya madini . Ni habari za kufurahisha ingawa bado taifa linategemea malipo mengi zaidi kutoka kwa makampuni hayo,”amesema.

Amesema hatua hiyo ya sasa ni msingi mkubwa na imara ambao umewekwa na rais Magufuli na kwamba kwenye vito vya thamani kama Almasi, Tanzanite kuna mengi ambayo nchi itafaidika nayo.

Katika hatua nyingine, ameipongeza Mamlaka ya Hali ya Hewa(TMA) kwa tahadhari ya uwezekano wa kuwepo kwa mvua itakayoleta madhara kama itanyesha kwa kiwango kilichotabiriwa.

“Hii ni hatua ya maendeleo kiteknolojia kwa idara hiyo, jambo linalowawezesha wale wanaoishi kwenye maeneo hatarishi kuweza kuchukua tahadhari mapema ili kulinda maisha na hali zao,”amesema.


Amesema wao huamini kuwa mvua za Mungu hazileti madhara kwa watu, kwani alishaapa baada ya gharika ya Nuhu hata iangamize  dunia kwa maji.

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search