Tafiti za kisayansi hupunguza magonjwa kwa asilimia 40...soma habari kamili na Matukio360..#share

Salha Mohamed
IMEELEZWA tafiti za kisayansi zikitumika vizuri hupunguza asilimia 40 ya magonjwa kwa binadamu

Katibu wa Chama cha watoa huduma za afya binafsi Dk. Rebeca John (kushoto) akisisitiza jambo kwa waandishi wa habari (hawapo pichani) kuhusu kongamano la nne la kitaifa la afya, katikati ni Rais wa chama hicho Dk. Omary Chillo na kulia ni Afisa Tawala wa chama hicho  Joseph Mhagama.
Hayo yameelezwa leo jijini Dar es Salaam na taasisi ya Tanzania Health Summit inayoratibu kongamano la Afya nchini, lengo likiwa kujadili changamoto za afya na kuboresha sekta hiyo.

Kongamano hilo linalotarajiwa kufanyika Novemba 14 na 15, 2017 katika  Ukumbi wa kimataifa za Mwalimu Nyerere(JNICC), litajadili juhudi za serikali na tafiti mbalimbali zilizofanywa na wanasayansi katika afya.

Kiongozi wa kongamano hilo, Dk Omary Chillo amesema mapendekezo  yanayoonesha suluhisho yatatolewa na kuandikwa vitabuni na kusambazwa kwenye  taasisi za afya na utekelezaji wake utafuatiliwa.

Amesema wanatarajia kupata wadau wa Afya takribani 500 kutoka ndani na nje ya nchi wakiwemo wataalamu wa Afya, watunga sera, watafiti wa magonjwa, wachumi, wazambazaji wa vifaa tiba na dawa, wawekezaji katika sekta ya Afya na wadau wote wa sekta hiyo.

Amesema watafiti mbalimbali watajadili na kutoa majibu ya tafiti zao kama walizofanya kwa panya kugundua magonjwa ambapo tafiti hizo zikitumika vizuri mtu anauwezo wa  kujikinga na magonjwa kwa asilimia 40.

Kwa upande wake Katibu wa Taasisi hiyo,Dk Rebecca John ametoa wito kwa wadau wa afya kutoka Serikalini, mashirika binafsi, hospitali, Asasi zisizo za kiserikali,taasisi za kitaalamu, watengenezaji wa bidhaa za afya, wazambazaji, wawekezaji na washiriki wa maendeleo kushiriki katika mkutano huu.

Kauli mbiu ya mkutano huo ni ‘Ni jinsi gani tunaweza kufikia malengo ya kuimarisha upatikanaji wa afya bora kwa kuunganisha tafiti za kisayansi, ubunifu na sera za afya huku mgeni rasmi akitarajiwa kuwa Mganga Mkuu wa Seriakali, Profesa Hashim Kambi.

           


About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search