Aveva, Kaburu waendelea kung'ang'aniwa...soma habari kamili na Matukio360..#share

 Na Abdulrahim Sadiki
JALADA la uchunguzi la kesi ya utakatishaji  fedha wa USD 300,000, inayomkabili rais wa klabu ya Simba, Evans Aveva na makamu wake, Godfrey Nyange ‘Kaburu’  bado lipo kwa mkurugenzi wa mashtaka ,(DPP).

 Rais wa klabu ya Simba, Evans Aveva  wa mbele na makamu wake, Godfrey Nyange ‘Kaburu’ 
Leo wakili mkuu wa serikali, Vitalis Peter ameeleza hayo kwa Hakimu Mkazi Mwandamizi, Victoria Nongwa na kuwa kesi hiyo ilipangwa kutajwa lakini  jalada la uchunguzi bado lipo kwa DPP. Ameomba kesi hiyo ipangiwe tarehe nyingine.

Hata hivyo wakili wa washtakiwa, Evodius Mtawala ameiomba mahakama iwasisitize upande wa mashtaka kuitilia mkazo kesi hiyo. Hakimu Nongwa ameahirisha kesi hiyo hadi  Novemba 10,2017.

Evans Elieza  Aveva na makamu wake, Geofrey wanakabiliwa na mashtaka matano ya kughushi, kuwasilisha nyaraka ya uongo na kutakatisha fedha USD 300,000.

Katika shtaka la kwanza, washtakiwa hao wanadaiwa kuwa  walikula njama ya kughushi fomu ya maombi ya kuhamisha fedha ya Machi 15,2016 wakionesha Klabu ya Simba inalipa mkopo wa  USD 300,000 kwa Evans Aveva wakati si kweli.

Katika shtaka la pili alidai kuwa Machi 15,2016 katika benki ya CRDB tawi la Azikiwe Ilala Aveva akijua alitoa nyaraka za uongo ambayo ni fomu ya maombi ya kuhamisha fedha ya Machi 15,2016 wakati akijua ni kosa.

Katika la tatu la kutakatisha fedha, Aveva na Nyange wanadaiwa kuwa kati ya Machi 15 na Juni 29,2016 Dar es Salaam  kwa pamoja walikula njama ya kutakatisha fedha kwa kupata USD 300,000 wakati wakijua ni zao la uhalifu.

Kwa upande wa shtaka la nne la kutakatisha fedha, Aveva anadaiwa kuwa kati ya Machi 15,2016 katika benki ya Baclays Mikocheni alijipatia USD 300,000 wakati akijua zimetokana na kughushi.

Katika shtaka la tano la kutakatisha fedha, mshtakiwa Nyange anadaiwa kuwa  Machi 15,2016 katika benki ya Baclays tawi la Mikocheni alimsaidia Aveva  kujipatia USD 300,000 wakati akijua fedha hizo zimetokana na kughushi. Washtakiwa wapo rumande kwa sababu shtaka la kutakatisha fedha linalowakabili halina dhamana.

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search