'UPDATES' Zitto, kamati kuu ACT waripoti Polisi....soma habari kamili na Matukio360..#share

Na mwandishi wetu
VIONGOZI wa chama cha ACT Wazalendo,  leo  wameripotia katika vituo viwili tofauti vya polisi jijini Dar es Salaam.

Kaimu katibu mkuu ACT Wazalendo, Dorroth Semu akifika katika kituo cha makosa ya uchunguzi wa kifedha eneo la Kamata

Saa nne asubuhi kaimu katibu mkuu wa ACT Wazalendo, Dorroth Semu na mwenyekiti, Yeremia Maganja wamewasili katika kituo cha makosa ya uchunguzi wa kifedha eneo la Kamata

Saa nne na nusu Zitto Kabwe akiwa na mawakili wawili amewasili kituo cha Chang’ombe kujua hatma kama atafikishwa mahakamani au uchunguzi dhidi yake bado haujakamilika.

Zitto anatuhumiwa kufanya makosa ya uchochezi huku kamati kuu ya ACT Wazalendo ikituhumiwa kwa kutoa takwimu za uchumi kinyume cha sheria na utaratibu.

Afisa Habari wa ACT Wazalendo, Abdallah Khamis ameiambia Matukio360 kuwa Zitto ameambata na mke wake  na baadhi ya viongozi wa chama hicho.

Huku kaimu mwenyekiti na katibu nao wameongozana  na mwanasheria  Michael Mboya.

Miongoni mwa makosa aliyoojiwa Zitto ni kwamba Jumapili ya  Oktoba 29, 2017 alipokuwa kwenye mkutano wa kuzindua kampeni za udiwani katika Kata ya Kijichi, Wilayani Temeke alitoa maneno yanayoweza kupelekea uvunjifu wa amani. Maneno hayo ni yafuatayo:

1. Kwamba wananchi wasiichague CCM kwa sababu Serikali yake imeshindwa kufanya uchunguzi na kuwakamata watu waliompiga risasi Mbunge Tundu Lissu mpaka siku hiyo.

2. Kwamba wananchi wasiichague CCM kwa sababu Serikali yake imeshindwa kueleza chanzo cha miili ya watu wanaookotwa kwenye fukwe za bahari kama Coco Beach. Hivyo kuichagua CCM ni sawa na kuwaunga mkono waliofanya vitendo vya kumshambulia Tundu Lissu na wanaoua watu wanaookotwa kwenye fukwe.




Kaimu katibu mkuu ACT Wazalendo, Dorroth Semu akipanda kwenda katika chumba cha mahojiano katika kituo cha makosa ya uchunguzi wa kifedha eneo la Kamata leo jijini Dar es salaam

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search