'UPDATES' Zitto Kabwe atakiwa kuripoti Polisi Ijumaa ijayo...soma habari kamili na Matukio360..#share
Na mwandishi wetu
JESHI
la Polisi limemtaka kiongozi wa Chama cha ACT Wazalendo, Zitto Kabwe kuripoti tena katika kituo cha Chang’ombe Ijumaa ya Novemba 17, 2017
Mbunge wa Kigoma Mjini, Zitto Kabwe
Alifika kituoni hapo mapema leo kufuatia wiki iliyopita kuhojiwa na Polisi akituhumiwa kufanya makosa ya uchochezi.
Alifika kituoni hapo mapema leo kufuatia wiki iliyopita kuhojiwa na Polisi akituhumiwa kufanya makosa ya uchochezi.
Akizungumza na Matukio360 mara baada ya kutoka kituoni hapo, Zitto amesema kinachosubiriwa ni jalada la maelezo kutoka kwa mkurugenzi wa makosa ya jinai (DCI) kwenda kituoani hapo na kwamba uenda hadi kufikia Ijumaa litakuwapo
Awali Afisa
Habari wa ACT Wazalendo, Abdallah Khamis ameiambia Matukio360 kuwa leo Zitto
akiambata na mkewe na baadhi ya viongozi wa ACT alifika ili kujua hatma kama atafikishwa mahakamani au uchunguzi
dhidi yake bado haujakamilika.
Miongoni
mwa makosa aliyohojiwa ni kwamba Jumapili ya Oktoba 29, 2017 alipokuwa kwenye mkutano wa
kuzindua kampeni za udiwani katika Kata ya Kijichi, Wilayani Temeke alitoa
maneno yanayoweza kupelekea uvunjifu wa amani. Maneno hayo ni yafuatayo:
1.
Kwamba wananchi wasiichague CCM kwa sababu Serikali yake imeshindwa kufanya
uchunguzi na kuwakamata watu waliompiga risasi Mbunge Tundu Lissu mpaka siku
hiyo.
2.
Kwamba wananchi wasiichague CCM kwa sababu Serikali yake imeshindwa kueleza
chanzo cha miili ya watu wanaookotwa kwenye fukwe za bahari kama Coco Beach.
Hivyo kuichagua CCM ni sawa na kuwaunga mkono waliofanya vitendo vya
kumshambulia Tundu Lissu na wanaoua watu wanaookotwa kwenye fukwe.
No comments:
Post a Comment