CCM ilimvua uanachama Nyalandu, Spika Ndugai athibitisha...soma habari kamili na Matukio360..#share

Na mwandishi wetu
OFISI ya Spika wa Bunge imesema Lazaro Nyalandu si mbunge tena na hatua stahiki za kuiarifu Tume ya Taifa ya Uchaguzi(Nec) zinaendelea kuchukuliwa.


Imesema hatua hiyo inafuatia katibu mkuu wa CCM kuiandikia ofisi ya Bunge barua ikimualifu kwa muda CCM ilishaanza kumchukulia hatua kiudhibiti na kinidhamu dhidi ya vitendo na kauli za Nyalandu zisizoridhisha kinyume na misingi, falsafa na itikadi ya chama hicho.

Hivyo kuanzia tarehe ya barua hiyo ya Oktoba 30, 2017 Nyalandu amepoteza sifa za uanachama wa CCM na kupoteza nafasi zote za uongozi wa ndani wa chama hicho na ubunge kwa mujibu wa ibara ya 13 ya CCM.


Hatua hiyo inafuatia baada ya hivi karibuni Nyalandu kutangaza kujiuzulu ubunge na kung’atuka CCM 

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search