Kesi 'Mpemba wa Magufuli' kuhamia mahakama ya mafisadi...soma habari kamili na Matukio360..#share

Na Abdulrahim Sadiki
KESI ya kujihusisha na biashara haramu ya meno ya tembo inayomkabili mfanyabiashara Yusuf Ali ‘Mpemba wa Magufuli’ na wenzake watano inatarajiwa kupelekwa katika Mahakama Kuu Kitengo cha Rushwa na Uhujumu Uchumi 'Mahakama ya Mafisadi'
Meno ya tembo

Wakili wa Serikali, Elizabeth Mkunde  ameyaeleza hayo leo  mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Thomas Simba. Hatua hiyo imefikiwa baada ya upande wa mashtaka kukamilisha upelelezi wa kesi hiyo. Hata hivyo kesi imeahirishwa hadi Novemba 15,2017.

Mbali ya Mpemba,  washtakiwa wengine ni Charles Mrutu, mkazi wa Mlimba, Morogoro, Benedict Kungwa, mkazi wa Mbagala Chamazi, Jumanne Chima, mkazi wa Mbezi, Ahmed Nyagongo, dereva na Pius Kulagwa.

Washtakiwa hao  wanakabiliwa na mashtaka manne ya kujihusisha na biashara ya meno ya tembo yenye thamani ya  milioni 785.6.

Inadaiwa katika tarehe tofauti kati ya Januari, 2014 na Oktoba, mwaka huu wakiwa Dar es Salaam, Tanga, Iringa na Mtwara, walijihusisha na mtandao wa ujangili kwa kukusanya na kuuza nyara za serikali ambazo ni vipande vya meno ya tembo 50 vyenye thamani ya Dola za Marekani 180,000 sawa na milioni 392.8 bila kuwa na kibali cha Mkurugenzi wa Wanyamapori.

Oktoba 26, 2016, washtakiwa hao wakiwa Mbagala Zakhem, walikutwa na vipande vya meno ya tembo10 vyenye   uzito wa kilo 13.85 vya thamani ya dola za Marekani 30,000 sawa na milioni 65.4

Wanadaiwa kuwa  Oktoba 27,2016 wakiwa Tabata Kisukuru washtakiwa hao walikutwa na vipande vinne vya meno hayo ya tembo yenye uzito wa kilo 11.1 na thamani ya dola za Marekani 15,000  sawa na milioni 32.7


Pia Oktoba 29,2016 walikutwa na vipande 36 vya thamani ya milioni 294.6  bila kuwa na kibali cha Mkurugenzi wa Wanyamapori.

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search