Diamond 'matatani' kuilipa Msondo Ngoma milioni 300...soma habari na Matukio360..#share

Na Mwandishi Wetu

BENDI ya Muziki wa Dansi ya Msondo Ngoma imeipa siku saba Kampuni ya Muziki wa Kizazi Kipya ya Wasafi Classic Baby (WCB) iliyoko chini ya msaani maarufu nchini,Naseeb Abdul ‘Diamond’ kuilipa milioni 300.
Mkurugenzi wa Kampuni ya Wasafi Classic Baby (WCB) Naseeb Abdul 'Diamond'.

Kwa mujibu wa barua iliyoandikwa na Mkurugenzi Mwenza wa Kampuni ya Uwakili ya Maxim Advocates, Mwesigwa Muhingo wanaoisimamia bendi hiyo ya Msondo Ngoma kwenda kwa Mkurugenzi wa WCB, imeeleza kuwa ni kutokana na wao kutumia melodi ya wimbo ‘ajali’ unaomilikiwa na Msondo Ngoma katika wimbo wa ‘Zilipendwa’ bila ruhusa.

Aidha barua hiyo imebainisha kuwa ikiwa WCB itashindwa kulipa fedha hizo ndani ya muda huo, hatua nyingine za kisheria zitafuata.


Wimbo wa zilipendwa uliimbwa na wasanii waliopo chini ya lebo hiyo ya WCB, ambao ni Diamond Platnumz, Rich Mavoko, Rayvanny, Queen Darlin, Maromboso na Lavalava.

Tayari baraza za sanaa (Basata) na lile la haki miliki(Cosota) wamethibitisha kupokea barua ya madai hayo kutoka kamouni ya uwakili ya Maxim


About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search