Dk Ndugulile: TFDA ongezeni 'spidi' katika utendaji ...soma habari kamili na Matukio360..#share

Na Abrahama Ntambara
NAIBU Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dk. Faustine Ndugulile ameitaka mamlaka ya chakula na dawa (TFDA) kuendeleza mapambano ya kudhibiti uingizwaji wa dawa duni, vifaa tiba na vitenganishi visivyo na ubora nchini.

Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dk. Fustine Ndugulile kushoto akiwa ameshikana mkono na Mkurugenzi Mkuu wa TFDA, Hiiti Sillo baada ya Uzinduzi huo jijini Dar es Salaam.

Pia ameitaka TFDA iendelea kuuboresha mfumo wa ubora wa huduma  kwa kutenga rasilimali za kutosha, ili kuhakikisha wanendelea kutoa huduma bora za udhibiti kwa kukidhi mahitaji na matarajio ya wateja, bila kuathiri ubora, usalama na ufanisi wa bidhaa wanazodhibiti.

Ameyasema hayo leo jijini Dar es Salaam  katika uzinduzi wa cheti cha Mfumo wa  Uhakiki Ubora wa Huduma kinachoendana na Kiwango cha Kimataifa cha ISO 9001:2015 ambacho  TFDA walitunukiwa na Shirika la ISO Agosti 2017 na ISO baada ya ukaguzi wa kina.

Mkurugenzi Mkuu wa TFDA Hiiti Sillo amesema  utekelezaji wa mfumo huo ni chachu ya maendeleo yaliyofikiwa na mamlaka hiyo.

Amesema Tanzania ni nchi ya kwanza kwa nchi za Afrika Mashariki kutumia mfumo huo katika kutoa huduma za wazi kwa wadau na wateja wake huku ikiwa ya pili kwa Afrika ikitanguliwa na Ghana.

“Mfumo huu sasa unatekelezwa katika Kurugenzi na Ofisi zote za Kanda za TFDA,” amesema Sillo.

Sillo amebainisha kuwa mfumo huo unajumuisha shughuli za kutengeneza, kufanya marejeo na kusimamia matumizi ya nyaraka, kufanya kaguzi za ndani kwa kutumia timu ya Wakaguzi wa Ndani wa Mifumo waliofuzu mafunzo ya ukaguzi.

Nyingine ni kusimamia ukaguzi wa Nje wa Mfumo kwa ajili ya kupewa cheti cha Usajilicha ISO, kuratibu marejeo ya mfumo yanayofanywa na Menejimenti pamoja na kutekeleza na kusimamia mfumo wa kusimamia vihatarishi (Risk Management Framework).


About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search