Muhimbili, Aga Khan kupandikiza matiti bure...soma habari kamili na Matukio360..#share

Na Salha Mohamed
HOSPITALI ya Taifa Muhimbili(MNH), Aga khan na taasisi isiyo ya kiserikali ya Women for Women  wanatarajia kufanya upasuaji na kuotesha matiti yaliyokatwa kutokana na saratani  pamoja na upasuaji kwa watoto walioungua, bure.

 Daktari bingwa wa upasuaji hospitali ya Aga Khan, Dk Aidan Njau akizungumza na waandishi wa habari kuhusu kuanza kwa upasuaji na kupandikiza matiti kwa wanawake waliokatwa kutokana na satarani, kulia ni Daktari bingwa wa upasuaji Hospitali ya Taifa Muhimbili, Dk. Edwin Mrema.

Upasuaji huo unaoanza leo utahusisha wagonjwa 40 wa kuanzia

Hayo yameelezwa leo jijini Dar es Salaam  na Daktari wa Bingwa wa Upasuaji Hospitali ya Aga khan, Dk Aidan Njau alipozungumza na waandishi wa habari kabla ya kuanza kwa upasuaji huo.

 “Mwanamke anapoambiwa anasaratani ya titi anapata maumivu makali na huathirika kisaikolojia hasa wanapoambiwa linatakiwa likatwe na wengine huacha na kuwaumiza  na  saratani husamba mwilini kisha  kufa,”amesema.

Amesema mwanamke aliyekatwa matiti anakuwa na maumivu zaidi pindi anaporudi kwenye jamii hujiona yupo tofauti na wenzake kimaumbile.

 “Mchakato huo utakuwa endelevu na wanawake ambao matiti yao yamekatwa wafike hospitali ili kupata matibabu kwa kuhamisha sehemu ya mwili na kuitengeneza iwe ziwa na ataendelea kama kawaida hata akivaa nguo itakaa sawa,”amesesma.

 Daktari bingwa wa upasuaji MNH, Dk Edwin Mrema amesema upasuaji huo ni mwendelezo wa hatua za mradi wa taasisi ya Women for Women na kwamba wanafanya upasuaji kwa wanawake na watoto waliopata ajali ya moto.

“Wagonjwa tuliowafanyia upasuaji wamepata mabadiliko wameweza kurudi kwenye jamii  awali walikuwa hawawezi kujichanganya kwenye jamii kutokana na kuungua moto,”amesema

Amesema ili kuendeleza upasuaji huo wametoa nafasi kwa wanafunzi wa chuo cha Aga Khan na Muhimbili (Muhas) ili kuwaongezea uwezo wa kufanya upasuaji kwa kushiriki katika upasuaji huo.



About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search