Hukumu kesi ya Lulu dhidi Kanumba leo...soma habari kamili na Matukio360..#share
Na Abdulrahim Sadiki
LEO
Novemba 13, 2017 Mahakama Kuu ya Tanzania inatarajia kutoa hukumu ya kesi ya
kuuwa bila kukusudia inayomkabili Elizabeth Michael 'Lulu'
Masnii wa filamu, Elizabeth Michael 'Lulu'
Hatua
hiyo itafuatia baada ya wazee watatu wa
Baraza kutoa ushauri wao kwa mahakama kwamba Lulu' ameua bila kukusudia au la.
Lulu
anakabiliwa na kesi ya kuuwa bila kukusudia, akidaiwa kumuuwa msanii mwenzake,
Steven Kanumba April 7, 2012.
Awali
kabla ya wazee kutoa maoni hayo, Jaji Sam Rumanyika alisoma maelezo ya ushahidi
wa pande zote mbili kisha kusikiliza maoni hayo.
Kabla
ya kutoa maoni hayo, Jaji Rumanyika alisema kimsingi ushahidi wa upande wa
mashtaka umejikita kwenye ushahidi wa kimazingira kwa sababu Lulu ndiye mtu wa
mwisho kuwa na Kanumba.
Alisema
ushahidi wa kimazingira unakuwa sio wa moja kwa moja, licha ya kuwa una vipande
mithili ya nyololo ambavyo vimeshikana.
"Hivyo
waungwana mkumbuke katika utoaji wa maoni yenu sio lazima mthibitishe makosa,
pia kama mkiona mshtakiwa hausiki basi msisite kuieleza mahakama,".
Akitoa
maoni yake, Mzee wa Baraza Omary Panzi amesema Lulu ameua bila kukusudia.
Amesema
kuwa hatua hiyo inatokana na ushahidi wa mdogo wake Kanumba, Seth Bosco ambaye
alielezea ugomvi uliotokea baina ya Lulu na marehemu.
"Maoni
yangu ni kwamba marehemu alikufa kwa sababu ya kuteleza ikizingatiwa ilikuwa ni
usiku na kulikuwa na giza, na chanzo cha kutekeleza ni ugomvi wake na
Lulu,".
Pia
Mzee wa pili, Bi.Sarah amesema Kanumba
alikufa kutokana na ugomvi ambapo ushahidi pia umetueleza kulikuwa na giza.
"
Hivyo Lulu hakuuwa makusudi bali aliuwa bila kukusudia, ".
Naye
Mzee wa Tatu, Rajabu Mlawa ametoa maoni yake alisema kutokana na sababu
zilizosomwa anaridhika na hakuna ubishi kuwa Lulu ana kosa la kuuwa bila
kukusudia.
"
Ameuwa bila kukusudia na nimeridhika na kilichosemwa, kwani Kanumba alikuwa na
mwili mkubwa na alikuwa katika hali ya kulewa, hivyo inaonekana katika heka
heka za ugomvi inawezekana Lulu alitumia nguvu kidogo ya kumsukuma Kanumba hadi
kudondoka,".
Baada
ya kutoa maoni hayo, Jaji Rumanyika alisema kuwa anatarajia kutoa hukumu ya
kesi hiyo leo Novemba 13/2017.
No comments:
Post a Comment