Jalada kesi ya Aveva na Kaburu lalejeshwa Takukuru..soma habari kamili na Matukio360..#Share

Na Abdulrahim Sadiki
JALADA la kesi  inayowakabili viongozi wa klabu ya Simba, rais  Evans Aveva na makamo wake Godfrey Nyage ‘Kaburu’ limerejeshwa Takukuru. Kwa muda mrefu sasa  lilikuwepo kwa Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP).

Rais wa klabu ya Simba, Evans Aveva wa mbele akiwa na Makamu wake, Godfrey Nyage'Kaburu' wakiingia katika moja ya chumba cha mahakama ya hakimu mkazi kisutu

Hayo yamesemwa leo mbele ya Hakimu Mkazi Mwandamizi, Mwambapa na Mwendesha Mashtaka wa Takukuru, Leonard Swai.

Swai amedai  jalada hilo limerudishwa  juzi Takukuru kutoka kwa DPP na ametoa maelezo  ya kukamilisha zaidi upelelezi.

Hayo yameelezwa na Swai,  baada ya Wakili wa Utetezi Philemon Mutakyawa kuuliza  juu ya jalada hilo lililokuwepo kwa DPP limefikia wapi.

Aveva na makamu wake wanakabiliwa na Mashtaka matano ya  uhujumu uchumi.

Ikiwamo ya kughushi, kuwasilisha nyaraka ya uongo na kutakatisha wa Dola za Marekani (USD) 300,000.

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search