TFF yatangaza kocha mpya Kilimanjaro Star, kutangaza kikosi chake kipya..soma habari kamili na Matukio360..#share

Na mwandishi wetu
SHIRIKISHO la mpira wa miguu nchini(TFF) limemtangaza kocha mpya wa timu ya soka ya Kilimanjaro Star itakayoshiriki mashindano ya Chaleji nchini Kenya.

Msemaji wa TFF, Alfred Lucas

Leo jijini Dar es Salaam afisa habari wa TFF, Alfred Lucas amemtangaza kocha huyo kuwa ni Ami koradi Minje ambaye atahusika na mashindano ya Chaleji tu.

‘Kocha huyu atahusika katika mashindano ya Chalenji tu, baada ya mashindano hayo kuisha timu itarudi kwa kocha mkuu, Salum Mayanga
,’’ amesema

Akizungumza katika utambulisho huo, Ami Minje amesema kesho atakitangza kikosi chake kitakachoshiriki mashindano hayo ambayo Kilimanjaro Star ipo kundi moja na wenzao wa Zanzibar Herroes.

‘Ningependa niulizwe maswali zaidi kesho(Novemba 18,2017) mara baada ya kutangaza kikosi cha Kilimanjaro Star kitakachoshiriki mashindano ya Chalenji  nchini Kenya,’’ amesema Minje

Hata  hivyo amesema amekuwa akifundisha soka nchini Uingereza kwa takribani miaka 13 na kwamba alikuwa akirejea nchini kusaidiana na kocha mkuu wa Taifa Star, Salum Mayanga

‘Nimekuwa nikifundisha soka katika chuo cha michezo ch Hall College  cha Uingereza na nina beji ya ufundishaji ya shirikisho la soka duniani (FIFA),’’ amesema


Mashindano hayo ya  Chalenji ya mwaka 2017 yanayoandaliwa na baraza la soka afrika mashariki( CECAFA) yatafanyika Kenya.

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search