Mchoro wa Yesu wauzwa dola milioni 450....soma habari kamili na Matukio360..#share

Na mashirika ya kimataifa
MCHORO wa miaka 500 wa Yesu unaoaminiwa kuchorwa na Leonardo da Vinci, umeuzwa mjini New York kwa dola milioni 450.

 Mchoro wa Yesu Salvator Mundi au (Mkombozi wa Dunia) umeuzwa dola milioni 450 Marekani

Mchoro huo unajulikana kama Salvator Mundi (Mkombozi wa Dunia). Ndio mchoro wa bei ya juu zaidi kuwai kuuzwa kwa mnada.

Hata  hivyo Simu ya Hitler iliuzwa dola 243,000 Marekani. Leonardo da Vinci aliyefarika mwaka 1519 ana michoro 20   iliyobaki.

Ni huo mmoja tu unaoaminiwa kuwa mikononi mwa mtu ambao unaamimiwa kuwa ulichorwa baada ya mwaka 1505.

Picha hiyo inamuonyesh Yesu akiwa ameinua mkono mmoja huku mwingine ukishika kioo.

Mwaka 1958 mchoro huo uliuzwa kwenye soko la mnada mjini London kwa Dola 60. Wakati huo mchoro huo uliaminiwa kuwa kazi ya mfuasi wa Leonardo na wala haukuwa wa Leonardo mwenyewe.


Miaka minne iliyopita mchoro huo ulinunuliwa na raia wa Urusi kwa dola milion 127.5 lakini wakati huo hakuuzwa katika mnada.

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search