Mahakama yapokea hati ukamataji mali za Wema ..soma habari kamili na Matukio360...#share
Na
mwandishi wetu
MAHAKAMA
ya Hakimu Mkazi Kisutu imepokea hati ya
ukamataji mali iliyojazwa katika upekuzi nyumbani kwa msanii wa filamu,Wema
Sepetu kama kielelezo. Mbali na Wema, wengine wanaokabiliwa na kesi hiyo ni Angelina Msigwa na Matrida Seleman Abbas.
Wema Sepetu kushoto akitinga Mahakamani
Kwa pamoja
wanakabiliwa na mashtaka mawili ya kukutwa na kiwango kidogo cha dawa za
kulevya na kutumia dawa za kulevya.
Hakimu
Mkazi Mkuu wa Mahakama hiyo, Thomas Simba ametoa uamuzi huo leo kwa kuwa
upekuzi huo ulifanywa nyumbani kwa Wema na si mwilini mwa Wema.
Amesema
upekuzi huo ungefanywa maungoni mwa Wema ni lazima apekuliwe na mwanamke.
Uamuzi
huo imefuatia baada ya upande wa
mashtaka ukiwakilishwa na Wakili wa Serikali, Constantine Kakula kuiomba
Mahakama ipokee hati hiyo ya ukamataji Mali kama kielelezo huku upande wa
utetezi ukiwakilishwa na Wakili Peter Kibatala ukipinga.
Hakimu
Simba ameahirisha kesi hiyo hadi Novemba 16,2017 na kwamba siku hiyo upande wa
mashtaka upeleke mashahidi wao wote.
Katika
upekuzi uliofanyika nyumbani kwa Wema inadaiwa ilikutwa misokoto inayodhaniwa kuwa ni dawa za kulevya
aina ya bangi.
Katika
ushahidi uliotolewa na Inspekta Msaidizi wa Jeshi la Polisi, Wille (43) kutoka
ofisi ya Mkuu wa Upelelezi wa Makosa ya
Jinai Kanda Maalum ya Dar es Salaam alidai
katika upekuzi huo walifanikiwa kukuta misokoto inayodhaniwa kuwa ni dawa za
kulevya aina ya bangi.
Wille
alidai Februari 4,2017 anaikumbuka kwa sababu aliitwa na Mkuu wake wa kazi na kupewa kazi ya kufanya upekuzi nyumbani kwa Wema na aliongozana na WP Mary,
Koplo Robert, PC Hassan na dereva kuelekea Unonio anapoishi Wema ili wakaufanye
upekuzi huo.
Inspekta Wille
alidai kuwa walipofika nyumbani kwa Wema huko Ununio waligonga
mlango na kwamba waliwakuta wasichana
wawili ambao ni wafanyakazi wa Wema na wakaomba
waitiwe mjumbe wa nyumba kumi Steven Noho wakaitiwa.
Shahidi huyo wa pili
wa upande wa mashtaka alidai kuwa walimueleza kuwa wamekwenda nyumbani kwa Wema
kwa nia ya kufanya upekuzi nyumbani kwa Wema na wanatafuta dawa za kulevya na
kitu chochote ambacho wangekitilia shaka.
Wema alisema dada
yake awepo ili ashuhudie upekuzi huo, dada yake alifika na tukapekuwa ambapo upekuzi wetu ulianzia jikoni ambapo juu ya kabati la vyombo tulifanikiwa kukuta msokoto mmoja unaodhaniwa
kuwa ni bangi na karatasi ya kusokotea, Alieleza shahidi huyo wa pili wa upande
wa mashtaka.
Katika chumba cha
Wema ambacho anahifadhia nguo na vitu vyake vingine mlango ulikuwa umefungwa
lakini wafanyakazi wake walituletea, tukafungua
na tukafanikiwa kukuta vipisi na msokoto unaodhaniwa kuwa ni bangi dirishani.”Alieleza shahidi
huyo wa pili wa upande wa mashtaka.
Akiendelea kutoa
ushahidi kwenye kesi hiyo, Inspekta Wille alidai kuwa upekuzi huo
uliendelea katika chumba cha wasichana
wa kazi wa Wema, walifanikiwa kukuta kiberiti ambacho ndani yake kulikuwa na
msokoto ambao unaonekana umeishavutwa.
Alidai kuwa baada ya
kufanya upekuzi huo, walisaini hati ya ukamataji wa mali ambapo yeye
aliisaini, Wema mwenye aliisaini,
wafanyakazi wake, dada yake, pamoja na mjumbe wa eneo la Unonio.
Aliongeza kuwa baada
ya hapo walienda kituoni na kumkabidhi mtunza vielelezo, Robert.
Inadaiwa kuwa
Februari 4,2017 katika Makazi ya Wema huko Kunduchi Ununio washtakiwa hao walikutwa na msokoto mmoja na
vipisi vya bangi vyenye uzito wa gramu 1.08.
Kwa upande wa Wema
yeye anadaiwa kuwa Februani Mosi, 2017 katika
eneo lisilojulikana jijini Dar es Salaam, alitumia dawa za kulevya aina ya Bangi.
Wema ni miongoni mwa
watu waliotajwa na Mkuu wa Mkoa Dar es Salaam, Paul Makonda wakituhumiwa
kujihusisha na dawa za kulevya.
Inadaiwa kuwa
Februari 3, 2017, Wema alijipeleka mwenyewe katika Kituo cha Polisi Kati ambapo
alikamatwa.
No comments:
Post a Comment