Kesi vigogo wa Tanesco kuunguruma Novemba...soma habari kamili na Matukio360...#share

 Na Abdulrahim Sadiki
KESI ya hujumu uchumi inayowakabili vigogo watano wa zamani wa Shirika la umeme nchini(Tanesco) na msambazaji kutoka kampuni ya M/S Young Dong Electronic Co. Ltd itaanza kuunguruma  Novemba 30, 2017.

Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu
Vigogo hao ni mkurugenzi wa Fedha, Lusekelo Kasanga, naibu mkurugenzi mkuu wa Tanesco, Robert Shemhilu, ofisa ugavi, Harun Mattambo,  mwanasheria wao, Godson Makia na msambazaji Martin Simba.

Wanashtakiwa kwa kuisababishia Serikali hasara ya milioni 275. Kesi hiyo itaanza kusikilizwa kwa ushahidi wa mashahidi wa upande wa mashtaka mbele ya  Hakimu Mkazi Mkuu wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Thomas Simba.

Washtakiwa hao wanakabiliwa na  mashtaka mawili  ya uhujumu uchumi ikiwamo matumizi mabaya ya madaraka na kusababisha hasara milioni 275.Upande wa Mashtaka unawakilishwa na Wakili Mkuu wa Serikali, Vital is Peter.

 Wanadaiwa  kati ya Januari na Desemba 2011 katika ofisi za Tanesco Ubungo, washtakiwa hao  wakiwa  waajiriwa wa shirika hilo, walitumia madaraka yao vibaya kwa kufanikisha malipo kwa msambazaji Martin Simba bila ya kufanya uhakiki.

 Imedaiwa  walifanya hivyo kinyume na kifungu cha 35 cha Sheria ya Manunuzi ya Umma namba 21  ya 2014 kitendo ambacho kilisababisha msambazaji huyo kupata faida.


Imedaiwa   kati ya Januari na Desemba, mwaka  2011 katika ofisi za Tanesco Ubungo, washtakiwa hao wakiwa waajiriwa wa shirika hilo pamoja na msambazaji huyo waliisababishia Serikali  hasara ya Sh 275,040,000. Washtakiwa hao wapo nje kwa dhamana.

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search