Kigamboni yaongoza kitaifa...soma habari kamili na Matukio360...#share

Na mwandishi wetu
HALMASHAURI ya manispaa ya Kigamboni imeongoza kwa kuwa ya kwanza kitaifa kati ya halmashauri 186 katika uwezeshaji wanawake nchini.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mh. Selemani Jafo (Katikati) akizungumza na wafanyakazi 

Hayo yamesemwa na Waziri wa Ofisi ya Rais TAMISEMI, Seleman Jafo wakati akizungumza na maafisa maendeleo ya jamii kutoka katika halmashauri zote nchini.

Hivi karibuni halmashauri ya manispaa ya Kigamboni imeonekana kufanya vizuri katika mambo mbalimbali ikiwemo kuingia katika kumi bora matokeo ya mtihani wa darasa la saba, kushika namba moja kwa Mkoa wa Dar es salaam katika masuala ya afya nk.

Wachambuzi wa mambo wanasema mafanikio hayo ya wilaya mpya nchini iliyoanza kufanya kazi Disemba 2016 yametokana na ushirikiano mzuri wa utendaji kazi na uwajibikaji uliopo miongoni mwa viongozi wa wilaya hiyo.
Mara kwa mara mkuu wa wilaya hiyo, Hashim Mgandilwa na mkurugenzi wa manispaa ya Kigamboni Stephen Katemba wameonekana wakiwa na ushirikiano thabiti ambao tija yake imeonekana katika mafanikio wanayoyapata licha ya wilaya hiyo kuwa mpya.

Aidha, balaza la madiwani, mbunge wa Jimbo la Kigamboni Mhe Dkt Faustine Ndungulile pia wameonekana kushikamana kwa kuweka mipango na mikakati ya pamoja ambayo imesaidia kupata mafanikio haya.

Baadhi ya wananchi wa Kigamboni kwa mara kadhaa wamekaririwa wakimshukuru rais Dk John Magufuli kwa namna alivyowapatia viongozi wachapa kazi wanaoendana na kasi ya Rais mwenyewe kwani kutenga kiasi cha pesa kwa ajili ya kuwawezesha kiuchumi limekuwa jambo la kuwakwamua na umaskini.

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search