Polisi wamsaka aliyenyuma 'mnunuzi' nyumba Lugumi...Soma habari kamili na Matukio360..#share

Na Abraham Ntambara

JESH la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam linamtafuta aliyemtuma Dk. Louis Shika (48) mkazi wa Tabata kuharibu mchakato wa uuzwaji wa nyumba za mfanyabiashara Said Lugumi kwa njia ya mnada ili kuweza kumfikisha katika vyombo vya sheria.


Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, SACP Lazaro Mambosasa akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam.

Hayo  yamebainishwa  leo  na Kamishna wa Polisi Kanda hiyo SACP Lazaro Mambosasa, akizungumza na waandishi wa habari, amesema jeshi hilo linamhisi mfanyabiashara huyo ndiye aliyemtuma kutokana na kudai kuwa fedha zitatoka Urusi huku ikijulikana  kuwa Lugumi aamekimbia nchini.

“Tunachoendelea kufuatilia ni kujua ni nani aliyemuajiri akazuie mnada kufanyika na kwa vyovyote vile ukitumia logic thinking ni kwamba mwenye kula hasara kama zitauzwa ni yeye mmiliki wa nyumba ambaye kimsingi alikwisha kimbia nchini,” amesema SACP Mambosasa

“Na huyu bwana kumbuka anasema fedha zinatoka Urusi na huyo bwana alikojificha anajua mwenyewe
Sasa huko Urusi inawezekana ndiko huyu mhalifu mweingine ambaye kimsingi anadaiwa na TRA, kwa hiyo kuna uhusiano, mtu yeyote mwenye busara yake atajua kwa nini huyu mtu ameingilia kuzuia mnada huu,” ameongeza.

SACP Mambosasa amebainisha kuwa kwa sasa kwa upande wa Dk. Shika, wanaendelea na hatua za upelelezi na pindi utakapokamilika jarada litakwenda kwa mwanasheria kwa ajili ya uandaaji wa hati ya mashtaka kwa ili mhusika kupelekwa mahakamani.

Tukio hilo lilitokea jana wakati wa mnada wa uuzwaji wa nyumba za mfanyabiashara huyo, mtuhumiwa huyo alishinda mnada huo kwa kutaka kununua nyumba zote tatu, nyumba moja ya Mbweni alitaka kununua kwa sh. bilion 1,200,000,000, nyumba ya pili Mbweni alishinda na alitaka kununua kwa sh. milioni 900,000,000 na nyumba ya tatu ya Upanga alishinda na kutaka kununua kwa sh. bilioni 1,200,000,000.

Lakini alipotakiwa kulipa fedha taslimu asilimia 25 ya mnada kwa kila nyumba, hakuwa na fedha ndipo alipokamatwa na jeshi hilo na kufukishwa kituoni  na upelelezi wa kesi hiyo unaendelea na mtuhumiwa atafikishwa mahakamani kwa hatua zaidi za kisheria.

Kwa upande mwingine SACP Mambosasa amesema wanamshikilia Willliam Lugita Jeremia (56) akijinadi ni wakili wa kampuni ya Faithfull Attorney Advocates huku akijua siyo wakili.

Amesema baada ya mahojiano mtuhumiwa amekiri kuwa si wakili ila aliwahi kusoma shahada ya sheria mwaka 2004 katika chuo Kikuu cha Dar es Salaam  na alikuwa mahakamani kuwakilisha wateja wake Nunu Muhamisy na wenzake katika MISC Application namba 9/2017 iliyokuwa inasikilizwa na Jaji Mahuru.
            
Pia mtuhumiwa ameeleza kuwa aliwahi kufanya kazi katika Fame ya Marando mwaka 2014 akiwa katika mafunzo ya vitendo na ameshawahi kusimamia kesi nyingi akiwa kama wakili.

Mtuhumiwa huyo alikamatwa jana akiwa katika Mahakama Kuu Kitengo cha Ardhi Mtaa wa Kivukoni kufuatia kitendo hicho, upelelezi wa kesi hiyo unaendelea na mtuhumiwa atafikishwa mahakamani kwa hatua zaidi za kisheria. 






About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search