Kigogo wa Takukuru apandishwa kizimbani...soma habari kamili na Matukio360..#share

Na Abdulrahim Sadiki

ALIYEKUWA Mhasibu wa Takukuru, Godfrey Gugai amefikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu na wenzake watatu wakikabiliwa na mashtaka 43 likiwamo la kumiliki mali ambazo hazina maelezo zenye thamani  bilioni 3.6 na utakatishaji wa fedha.


Akisoma hati ya mashtaka leo kwa Hakimu Mkazi Mkuu,Thomas Simba, Wakili wa Serikali, Wankyo Simon aliwataja washtakiwa wengine kuwa ni George Makaranga, Leonard Alloys na Yasini Katera.

Washtakiwa hao wanakabiliwa na shtaka moja la kumiliki mali ambazo hazina maelezo, kughushi 22 na 20 ya utakatishaji wa fedha.

Amedai kuwa kati ya Januari 2005 na Disemba 2015 Dar es Salaam Godfrey akiwa mtumishi wa Umma aliyeajiliwa na Takukuru alikuwa na mali ambazo hazina maelezo zenye thamani ya Sh 3,634,961,105.03 ambazo haziendani na kipato chake cha sasa na cha nyuma ambacho ni Sh 852,183,160.46.

Imedaiwa kuwa mshtakiwa huyo alipotakiwa kutoa maelezo ambayo yanaridhisha kuhusiana na yeye kumiliki mali hizo, alishindwa kutoa.

Wankyo amedai kati ya Januari na Juni, 2016  Dar es Salaam, Gugai  akishirikiana na wenzake walighushi mikataba ya mauziano akionesha ameuza Mali zake kwa wenzake na watu wengine wakati akijua siyo kweli.

Gugai anadaiwa kuwa  Agosti 14, 2009 alighushi mkataba wa mauziano akionesha kuwa   alimuuzia  Zena Mgallah plot  namba 225 block 6 Mbweni JKT,  wakati akijua si kweli.

Amedai kuwa Julai 5,2011 alighushi akionyesha  kumuuzia Salehe Sas plot namba 621,622 na 623 block A vilivyopo Gomba Arumeru.

Oktoba 20,2013 alighushi akionesha alimuuzia  Arif Premji plot namba 64  kilichopo Onunio Kinondoni.

Desemba 20, 2014  alighushi akionesha alimuuzia Edith Mbatia plot namba 737 block C kilichopo Mwambani Mwarongo Tanga  plot namba 1,2 na 3.

Gugai na George  Novemba 20,2009 walighushi wakionesha Gugai alimuuzia George plot namba 150 block 8 kilichopo Bunju Kinondoni.

Gugai na Leonard wanadaiwa kuwa Novemba 19 ,2009, Gugai walighushi wakionesha alimuuzia Leonard plot namba 275,277,296 na 297 block 2 zilizopo Nyamongo, Mwanza.

Washtakiwa hao,Gugai na Leonard Agosti 20,2010 Gugai walighushi wakionesha alimuuzia Leonard plot namba 90 block5 Bugarika Kwanza.

Wanaendelea kudaiwa  Septemba 10,2013 walighushi wakionesha Gugai alimuuzia Leonard  plot namba 713 block B Kiseke Mwanza na  Oktoba 20,2015 akionesha kumuuzia plot namba 230.

Gugai Novemba 30,2011 wanadaiwa kughushi hati ya makubaliano ya umiliki wa kiwanja akionesha  kumuuzia Manwali Masalakulangwa plot namba 14 block J Bunju na Novemba 15,2015 plot namba 103 na 104 Block L Bagamoyo.

Gugai Novemba 19,2015 wanadaiwa kughushi akionesha alimuuzia Masalakulangwa plot namba 184 block B Buyuni Temeke na Novemba 4, 2011 akionesha kumuuzia Rose Abdallah plot namba 34 block K , B Centre Dodoma.

Iliendelea kudaiwa kuwa Desemba 5,2013 alighushi  akionesha kumuuzia Rose Abdallah plot namba 32 block N, Itega Dodoma, Novemba 14, 2014 plot namba 47 block B kilichopo Mwongozo Temeke  na Novemba 30,2014 plot namba 24 na 39 block B na M vilivyopo Chidachi na Itega Dodoma.

Gugai Septemba 2015 anadaiwa kughushi akionesha alimuuzia Patrick Magesa plot namba 7/9 na 11/13 block C vilivyopo Mwakidila Magaoni Tanga, Oktoba 15,2015 plot namba 18 block J Mwarongo Tanga.

Iliendelea kudaiwa kuwa Gugai anadaiwa kughushi akionesha Desemba 22,2015 alimuuzia Yasin Katera plot namba 438 block D kilichopo Nyegezi Mwanza.

Desemba 22,2015 Gugai anadaiwa kumuuzia Yasini Katera plot namba 439 block D Nyegezi Mwanza.

Kuanzia shtaka la 23 hadi  43 washtakiwa hao wakabiliwa na Mashtaka ya utakatishaji wa fedha.

Anadaiwa kuwa kati ya Januari na Juni, 2016 Dar es Salaam kwa njia ya udanganyifu kwa lengo la kuficha umiliki wa Mali hizo kwa kuonesha zinamilikiwa na watu tofauti tofauti wakati akijua si kweli na ni mazao ya Rushwa ambayo yametokana na kosa la  kumiliki Mali bila maelezo.

Baada ya washtakiwa hao kusomewa mashtaka hayo waliyakana na Wankyo alidai kuwa upelelezi bado haujakamilika na kwamba tarehe ijayo wataeleza hali ya upelelezi.

Baada ya kueleza hayo,
 wakili Alex Mgongolwa akishirikiana na wakili  Semi Malimi walidai kuwa  wamejiridhisha shtaka la 23 hadi 43 ya utakatishaji wa fedha  hayakidhi vigezo vinavyotakiwa kwa makosa ya utakatishaji wa fedha.

Mgongolwa alidai kwa kuwa makosa hayo ya utakatishaji fedha hayaelezi kosa husika hats kidogo aliomba mahakama iyafutilie mbali chini ya kifungu cha 129 cha makosa ya Jinai ama mahakama nitumie mamlaka yake ya asili kuyafuta.

Kwa kuwa ili liwe kosa la utakatishaji fedha ni lazima kuwepo na kosa tangulizi, limefanyika na kupelekwa kupatikana kwa fedha, unachukua fedha hizo ama kujengea na ukauza  kuanzisha kitu kingine.

Mgongolwa alidai kuwa katika Mashtaka yanayowakabili wateja wake hayazungumzii fedha na fedha ndiyo msingi wa shtaka la utakatishaji fedha na kwamba katika kesi hiyo kinachojitokeza ni alidanganya Mali ya Fulani wakati siyo.

Mashtaka hayo hayana kabisa uhusiano na utakatishaji wa fedha na kwamba makosa hayo hayana dhamana ni lazima umakini katika tafsiri yake uwe wa  hali ya juu.


Kwa mapungufu hayo shtaka la 23 hadi la 43 hayana nafasi ya kusimama mbele ya mahakama yafutiliwe mbali.

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search