Tanzania kutoa tuzo za Pan African....soma habari kamili na Matukio360...#share

Na Abraham Ntambara

RAIS na Mwenyekiti wa baraza la Mapinduzi  Zanzibar Dk. Ali Mohamed Shein anatarajiwa  kuwa mgeni rasmi katika mkutano wa kimataifa wa masuala ya kidiplomasia na maendeleo ya kijamii.

Katikati ni mratibu wa mkutano wa kimataifa wa masuala ya kidiplomasia na maenedeleo ya kijamii kutoka YUNA, Selemani Kitenge.

Mkutano huo unatarajiwa kufanyika Novemba 18, 2017 jijini Dar es Salaam. Pamona na mambo mengine kutatolewa tuzo kwa mashirika na wadau mbali mbali, tuzo hizo zinajuliakana kama Pan African Humanitarian Summit and Awards 2017.

Akizungumza na waandishi wa habari leo  jijini Dar es Salaam Mratibu wa Mkutano huo Selemani Kitenge kutoka Asasi ya Vijana wa Umoja wa Mataifa nchini (YUNA),  amesema Tanzania imepewa heshima kwa mara ya kwanza kuandaa mkutano huo.

“Dhumuni la mkutano huu ni kutambua jitihada mbali mbali zinazofanywa na wadau barani Afrika ili kuendeleza na kudumisha amani na maendeleo ya Afrika,” amesema Kitenge.

Aidha amesema mkutano huo utawaleta pamoja wanadiplomasia, wadau wa maendeleo, vijana madhubuti kutoka nyanja mbali mbali barani Afrika na viongozi wa serikali ili kuajdili mustakabali wa dhima kuu ya mkutano wa mwaka huu utabebwa na kauli mbiu ya ya ‘Amani inewezekana Jana, Sasa na Kesho’.

Kitenge alitaja vipengele viwili  muhimu katika tuzo hizo kuwa ni Rafiki wa Afrika, tuzo ambazo watapewa watu wasio wakazi wa bara la Afrika ambao wamekuwa wakichangia maendeleo barani humu.

Amesema kipengele kingine ni tuzo ya Ujenzi wa Taifa na Amani ambayo watapewa watu wenye mchango katika ujenzi wa amani barani Afrika.

Pan African Humanitarian Summit and Awards zilianza toka mwaka 2015 na kufanyika nchini Ghana na mwaka 2016 zilifanyika nchini Dubai. Tanzania inakuwa nchi ya pili Afrika kuandaa mkutano huu.



About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search