Kishoka 'TRA' akamatwa...soma habari kamili na Matukio360..#share
MAMLAKA ya Mapato Tanzania (TRA) Novemba 03, 2017, ilifanikiwa kumkamata, Dunia Athumani Tema
mkazi wa Buguruni, Dar es Salaam kwa tuhuma za kujifanya Mtumishi wa TRA na kutoa
huduma kwa mteja ndani ya Ofisi ya TRA Kariakoo – Gerezani Jijini Dar es
Salaam.
Mkurugenzi wa Huduma na Elimu kwa Mlipakodi wa Mamlaka ya Mapato Tanaznia (TRA), Richard Kayombo.
Mara baada ya kukamatwa mtuhumiwa huyo alifikishwa
katika Kituo cha Polisi kilichopo Msimbazi, Dar es Salaam na kufunguliwa
RB ya
MS/RB/9263/17,
KOSA: KUJIFANYA MTUMISHI WA UMMA (TRA).
Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) inatoa
wito kwa wananchi wote kutoa taarifa mara moja katika Vituo vya Polisi vilivyopo karibu, Ofisi za TRA zilizopo karibu au
kupiga simu namba 0800780078 au 0800750075 endapo watakuwa na mashaka
na mtu yeyote anaye wahudumia.
na mtu yeyote anaye wahudumia.
Pia Mamlaka inawasisitiza wananchi wasikubali
kupewa huduma zozote na mtu wanayemtilia mashaka.
TRA inapenda kuwakumbusha kwamba,
watumishi wake wote wanapaswa kuvaa au kuwa na kitambulisho chenye majina
na cheo wanapokuwa wanatimiza majukumu yao ya kila siku mahali popote.
‘Pamoja Tunajenga Taifa Letu’
Imetolewa na;
Imetolewa na;
Idara ya Huduma na Elimu kwa Mlipa kodi
Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA)
Makao Makuu.
12/11/2017.
No comments:
Post a Comment