Trump, Kim Jong-Un watunishiana misuli...soma habari kamili na Matukio360..#share

VITA vya maneno baina ya Rais wa Marekani Donald Trump na Korea Kaskazini Kim Jong-Un vimerejelea tena kufuatia mpango wa nyuklia wa Korea Kaskazini.
Rais wa Marekani Donald Trump (Kushoto) na Rais wa Korea Kaskazini Kim Jong-un (Kulia)
Wizara ya mashauri ya nchi za kigeni ya Korea Kaskazini imemuita  rais Donald Trump kuwa "mchochezi wa vita na mzee" na kusisitiza kuwa haiwezi kamwe kuachana na mipango yake ya nyuklia.
Rais Trump alijibu kwa kuandika katika mtandao wake wa kijamii wa Tweeter kuwa, anashangaa ni kwa namna gani Kiongozi wa Korea Kaskazini anamuita mzee.
Kwa maneno yake, rais Trump amesema kuwa hatamuita Rais Kim Jong-un, kuwa mtu "mfupi na mnene".
Alisema kuwa atajaribu siku moja kuwa rafiki wa karibu wa rais huyo wa Korea Kaskazini.
Trump awali alimkejeli kiongozi huyo mkuu wa Korea Kaskazini, kwa kumuita mwendawazimu na 'mtu wa kuunda zana za roketi'.


About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search