Wazazi wanafunzi wajawazito kuswekwa rumande saa 48...Soma habari kamili na Matukio360..3#share

WAKUU wa wilaya na shule mkoani Rukwa wameagizwa kuwakamata na kuwaweka ndani kwa saa 48 wazazi wa wanafunzi watakaopewa ujauzito.
Agizo hilo limetolewa na Mkuu wa Mkoa huo Joachim Wangabo, baada ya kusomewa taarifa ya Shule ya sekondari Kirando, wilayani Nkasi iliyobainisha wanafunzi saba kupata ujauzito kwa kipindi cha Januari hadi Oktoba, 2017.

Amesema kumekuwepo na tabia ya kumalizana kienyeji na matokeo yake watuhumiwa kutofikishwa  sehemu husika ili waweze kuwajibishwa.

“Mwalimu mkuu unapogundua mwananfunzi ana mimba mweke pembeni ita wazazi wake, washirikishe polisi wawachukue wawekwe ndani kwa muda wa saa 48 hadi hapo watakapomtaja Muhusika wa mimba hiyo, ukifanya hivyo mara kadhaa mabadiliko yatatokea,” amesisitiza
Aidha amezitaka shule zote atakazo tembelea katika ziara yake ya kujitambulisha, zihakikishe zinabainisha hatua zilizochukuliwa dhidi ya watu wanaotuhumiwa kuwajaza wanafunzi ujauzito.

Mkuu huyo wa mkoa alikuwa ametembelea shuleni hapo kwa ajili ya kukagua ujenzi wa maabara na kuongea na wanafunzi.

Kwa upande wake Mwalimu Mkuu wa Shule hiyo Erneo Mgina, amesema kati ya wanafunzi saba waliopata ujauzito wanafunzi watatu ni wa “A – Level” na wanne ni wa “O – Level” na kueleza kuwa wengi wao hupata mimba wakati wa likizo na huwabaini pale tu wanaporudi shule na kuwapima.


About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search