Kitilya, wenzake waendelea kusota rumande...soma habari kamili na Matukio360..#share

Na mwandishi wetu
HARRY  Msamire Kitilya ambaye ni mwenyekiti wa kampuni inayoshughulikia  uwekezaji wa mitaji na dhamana (Egma) na waliokuwa maofisa wa benki ya Stanbic, Shose Mori Sinare na Sioi Graham Solomon wanaendelea kusota rumande kutokana na upelelezi wa kesi inayowakabili  bado haujakamilika.

Harry Kitilya katika akiwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu
Leo wakili wa serikali mwandamizi, Mutalemwa Kishenyi amedai mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Godfrey Mwambapa  kuwa upelelezi wa kesi hiyo bado haujakamilika. Pia amedai  bado wanasubiri awamu ya pili ya upelelezi kutoka nchini Uingereza.

Hakimu Mwambapa ameahirisha kesi hiyo  hadi Novemba 10, 2017 kwa ajili ya kutajwa ili kuangalia kama upelelezi utakuwa umekamilika ama la.

Kesi hiyo inasikilizwa na Hakimu Mfawidhi wa mahakama hiyo, Cyprian Mkeha.

Awamu ya kwanza ya vielelezo hivyo  kutoka nchini Uingereza  vimepokelewa na vinasubiriwa vya awamu ya pili.
Washtakiwa hao wanakabiliwa na mashtaka ya kula njama, kujipatia fedha kwa njia ya udanganyifu na kutakatisha fedha.

Wanadaiwa kutenda makosa hayo kati ya Machi 2013 na Septemba 2015 wakati wa mchakato wa mkopo wa dola za Marekani  milioni 550   kwa  serikali ya Tanzania kutoka Benki ya Standard Uingereza.

Wanadaiwa kuwa  Machi 2013 jijini Dar es Salaam walijipatia Dola za Marekani milioni 6  wakionyesha kuwa fedha hizo zilikuwa ni malipo ya ada ya uwezeshaji upatikanaji wa mkopo  na zililipwa kupitia  Kampuni ya Egma T Ltd.

Washtakiwa  hao wanadaiwa  kutakatisha fedha kwa kuhamisha, kuchukua na kuweka kiasi cha Dola za Marekani milioni 6  katika akaunti tofauti tofauti  za benki.

Kati ya  Machi 2013 na Septemba 2015, wanadaiwa  kuwa waliweka pesa hizo katika akaunti mbalimbali zilizomilikiwa na kampuni ya Egma na kwamba walipaswa kufahamu kuwa pesa hizo ni mazao ya uhalifu wa kughushi.



About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search