Okwi awahakikishia Simba ubingwa...Soma habari kamili na Matukio360...#share


NA MWANDISHI WETU

STRAIKA  wa Simba, Emanuel Okwi amewaambia mashabiki wa timu hiyo wasiwe na wasiwasi na ubingwa kwani anamini taji la Ligi Kuu Tanzania Bara msimu huu litatua Msimbazi.

Emanuel Okwi

Mshambuliaji huyo raia wa Uganda alisema alitoa kauli hiyo mara baada ya kumalizika kwa mchezo ambao Simba iliibuka na ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Mbeya City juzi Uwanja wa Sokoine Mbeya.

Ushindi huo uliirejesha Simba katika uongozi wa ligi na kuishusha Azam iliyoichapa Ruvu Shooting bao 1-0 Jumamosi iliyopita katika nafasi ya pili kutokana na kigezo cha tofauti ya mabao ya kufunga na kufungwa licha ya timu hizo kulingana pointi 19.

Akizungumza jijini hapa,Okwi amesema ushindi walioupata umewazidishia morali ya kuendelea kufanya vizuri ili hatimaye

"Lengo lilikua kupata ushindi ugenini haijalishi tumechezaje, tumefanikiwa kupata alama tatu ndio muhimu kwetu.

“Kurejea kwetu kileleni kumezidisha kiu yetu ya kuchukua ubingwa msimu huu,nawaomba mashabiki wa Simba waendelee kutuunga mkono na sisi tunapambana kwaajili ya kuwapa furaha,”alisema Okwi.


About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search