Makalla apiga marufuku ununuzi wa migomba shambani..soma habari kamili na Matukio360..#share

Na mwandishi wetu
MKUU wa mkoa wa Mbeya, Amos Makalla amepiga marufuku ununuzi wa migomba ikiwa shambani kwa kuwa inapunguza kipato kwa wakulima.

Mkuu wa mkoa wa Mbeya  Amos Makalla kulia akizungumza na mfanyabishara wa ndizi Sophia Mwakyusa  kushoto alipotembelea katika soko la muda la  Kiwira Wilayani Rungwe mkoani Mbeya .

Pia amesema ujenzi wa soko la kimataifa la zao  la ndizi unatarajiwa kujengwa mwakani na eneo limepatikana.

Amesema hayo alipokuwa akijibu hoja zilizotolewa na wakulima wa zao hilo wilayani Rungwe na kwamba wafanyabiashara wanapaswa kununua mkungu wa ndizi uliokomaa.

 “Pamoja na mambo mengine nataka wafanyabiashara kuacha  tabia ya kununua ‘kuchumbia’ migomba shabani hii ni changamoto inayosababisha wakulima kutonufaika na zao hilo. Wanunue mkungu wa ndizi uliokomaa na vinginevyo,” amesema na kuongeza

“Miongoni mwa utekelezaji wa vipaumbele ambayo tumejiwekea hapo mwakani  ni  ujenzi wa soko la kimataifa la zao la ndizi,  eneo linalokidhi vigezo kwa ajili ya mradi huo limepatikana.”

 Awali wakulima wa ndizi waliitaka  serikali kuharakisha ujenzi wa soko hilo  ili kufungua fursa za kiuchumi na thamani ya zao hilo kutokana na kukosekana kwa soko la uhakika

Wakizungumza na  kwa nyakati tofauti na  Matukio 360 wamesema zao limeshuka thamani kwa kiasi kikubwa hadi  baadhi ya wafanyabishara kununua kwa bei ambayo hailingani na gharama za uzalishaji.

 Mkulima, Amos Joseph amesema endapo serikali ikikamilisha  mradi huo kuna uwezekano mkubwa wa  mapato na uchumi wa wilaya ya Rungwe kukua.

"Ukosefu wa soko la zao ndizi ni changamoto inayosababisha kuuza kwa bei ya hasara. Mkungu mmoja tunauza kwa bei ya sh 2,000
hadi 4,000 kulingana na ukubwa,"amesema.

Naye Sophia Mwaikambo amesema pia halmashauri inapoteza mapato kutokana na kutokuwapo kwa soko la uhakika la zao hilo





About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search