Makonda azidi kupambana na wauza dawa...soma habari kamili na Matukio360..#share
Na
mwandishi wetu
MKUU wa mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda
amewataka mabaharia nchini kuisaidia serikali kwa kutoa taarifa za dawa za kulevya na mali za magendo zinazopitishwa na kuingia bila kufuata utaratibu hasa baharini.
Mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda
Ametoa
wito huo leo jijini Dar es Salaam alipokuwa akifungua Mafunzo ya Sheria ya Kazi
kwa mabaharia ya mwaka 2006 na Marekebisho
yake “Maritime Labor Convention 2006 as amended” kwa Chama cha Mabaharia Tanzania (TASU).
Katika
ukanda wa Kiuchumi wa Bahari, Makonda amewaahidi mabaharia hao wazawa kuwa
atahakikisha wanapata upendeleo wa kupata
ajira katika Ukanda wa Kiuchumi wa Bahari ili waweze
kusaidia kutoa taarifa zinazohusiana na dawa za kulevya ama mali za
magendo zinazopitishwa bila ya kufuata
utaratibu .
Pia
amewaaeleza wananchi kuwa wana haki ya kudai haki ya maendeleo ila kwa wale tu wanaolipa kodi
na atakapokutana na rais Magufuli wakati
akimpa taarifa za mkoa wa Dar es Salaam atampatia taarifa hizo na za chama hicho cha TASU.
Makonda
amesema hayo baada ya Baharia, Aloyce
Mpazi kusoma risala kwa niaba ya TASU
ambapo imepongeza kutambuliwa kwa vyeti vya mabaharia wahitimu wa Chuo
cha Bahari Dar es Salaam (DMI) na kwamba
hiyo inawasaidia mabaharia kupata fursa
ya kutambuliwa, kuajiriwa na kufanya kazi duniani kote.
Pia
inasaidia kupanuka kwa wigo wa ajira kwa mabaharia wa kitanzania ndani na nje
ya nchi na kuongezeka na kukua kwa
biashara ya bahari (Shipping Business) katika nchi yetu hasa shughuli za
bandari na wadau wake.
Mpazi
alidai kuwa hayo yanayotokana na serikali ya Tanzania kuhakikisha inaibakisha
Tanzanika katika orodha ya shirika la bahari duniani (Internatinal Maritime
Organization - IMO) ya nchi zilizokidhi mabadiliko ya matakwa ya sheria ya
mafunzo kwa mabaharia, Standard Training and Certification of Watch Keeping
(STCW 2010), Manila amendment” maarufu kama “IMO White List”.
Amesema kuishi kibaharia ni kudumisha miiko na
maadili ya kibaharia na kwamba hiyo imechangia kwa njia moja au nyingine
kuifanya Tanzania iwemo kwenye “White List” ya IMO.
Kwa
takwimu za usafirishaji za dunia zinaonesha kuwa zaidi ya 98% ya shehena kubwa
na nzito kutoka sehemu moja kwenda nyingine duniani zinategemea uchukuzi kwa
njia ya maji.
Takwimu
hizi zinadhihirisha jinsi ambayo fani ya ubaharia ilivyo na fursa pana za ajira
kwani uchukuzi huu unafanywa kwa njia ya meli zinazosafiri kuunganisha mabara
yote duniani.
Hii inamaanisha kuwa mabaharia wanahitajika
sana si tu hapa nchini lakini zaidi duniani kote, hasa kwenye nchi zenye
makampuni makubwa ya meli.
Hivyo
chama hicho kina kazi ya kuwakusanya mabaharia Tanzania nzima, kuwahimiza
wajiunge katika chama na kuwalea katika misingi na maadili ya kibaharia ili
kulinda na kuhifadhi sifa nzuri ambayo ndiyo silaha kubwa ya kuiweka nchi yetu
katika rekodi bora ya uchukuzi kwa njia ya maji na hivyo kuzidi kuweka
mazingira mazuri kwa mabaharia wetu kupata ajira kwa wingi.
Kwa
kuwa nchi ambazo mabaharia wake wanatuhumiwa kwa ukosefu wa maadili,
kusababisha au kuhusika katika ajali za majini mara kwa mara na matatizo
mengine yanayofanana na hayo, nchi hizo hupata shida sana mabaharia wake kupata
ajira katika meli hasa za kimataifa ambazo mishahara yake ni mikubwa.
I mac really excited about Tom Servo and Crow. They are hilarious! Thank you for featuring Hero Lost today. Star Wars will always be a big influence for me. I think Empire Strikes Back was the first movie I ever saw in the theater. Have a great week Alex :) Soma delivery
ReplyDelete