Malkia pembe za ndovu alalamika mahakamani...soma habari kamili na Matukio360..#share
Na Abdulrahim Sadiki
RAIA wa China Yang Feng Glan ‘Malkia wa Pembe za Ndovu’, ameilalamika Mahakama ya
Hakimu Mkazi Kisutu dhidi ya mashahidi wa upande wa mashtaka kutofika mahakamani.
Yang amelalamika leo mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Huruma
Shaidi akidai Jaji Mkuu ameagiza kesi za muda mrefu lazima zimalizwe mwaka huu.
" Rais Magufuli anasema hapa kazi tu, Nikasema
sasa mahakama ile kazi haipo kwa haraka, nipo mahabusu naumwa moyo najitahidi
nakuja," ameeleza Yang.
Ameomba mashahidi katika kesi hiyo wafike na si kila
siku kutoa udhuru wa kuumwa.
Yang aliyaeleza hayo baada ya Wakili Wankyo Simon
kudai kuwa shahidi waliyemtarajia kutoka ushahidi katika kesi hiyo bado anaumwa
na akaomba ipangiwe tarehe nyingine na kwamba siku hiyo wanaamini atakuwa
vizuri.
Wakili wa utetezi, Nehemiah Nkoko, aliomba mahakama
iliangalie hilo na kuwa waendelee na mashahidi wengine wa upande wa Mashtaka
ili kuokoa muda.
Wakili Wankyo alidai kuwa
katika hali ya kawaida ni lazima shahidi huyo amalizie kutoa ushahidi wake.
Hakimu Shaidi aliutaka
upande wa Mashtaka kupelekwa mashahidi
kama huyo hatakuwa hajatengemaa.
Kesi hiyo itaendelea kusikilizwa Novemba
21,24,27,28,29,30 na Desemba Mosi, 2017.
Washtakiwa wengine wanaokabiliwa na kesi hiyo ni
Salvius Matembo na Philemon Manase ambao kwa pamoja, wanadaiwa kuwa kati ya Januari Mosi, 2000 na Mei
22,2014 walijihusisha na biashara ya nyara za serikali.
Katika kipindi hicho washtakiwa hao wanadaiwa kufanya
biashara ya vipande 706 vya meno ya Tembo vyenye uzito wa kilogramu 1889 zenye
thamani ya Sh 13 bilioni bila ya kuwa na
leseni iliyotolewa na Mkurugenzi wa Wanyama Pori.
Wanadaiwa kuwa kati ya Januari Mosi, 2000 na Mei
22,2014 kwa makusudi raia wa China,
China, Yang Feng Glan aliongoza na
kufadhiri vitendo vya kijinai kwa kukusanya na kusafirisha vipande hivyo 706
vya Meno ya Tembo bila ya kuwa na kibali chochote kile kutoka kwa Mkurugenzi wa
Wanyama Pori.
Kwa upande wa washtakiwa Salvius na Manase wanadaiwa
kuongoza makosa ya uhujumu uchumi kwa kusaidia biashara ya nyara za serikali
kwa kukusanya, Kusafirisha na Kuuza Meno ya Tembo kwa nia ya kujipatia faida.
Ilidai kuwa Mei 21, 2014 katika eneo la Sinza
Palestina wilaya ya Kinondoni mshtakiwa Manase alitoroka chini ya ulinzi halali
wa askari wa Jeshi la Polisi D 7847 Koplo Beatus ambaye alikuwa akimshikilia
kwa makosa ya kujihusisha na biashara za nyara za serikali.
No comments:
Post a Comment