Serikali kusimamia sera kulinda watoto ...Soma habari kamili na Matukio360...#share


Na Abrahama Ntambara

SERIKALI itaendelea kusimamia sera za kulinda watoto  ili kuhakikisha wanakuwa katika makuzi mema hususani kwenye  lishe, elimu na dhidi ya vitendo vya ukatili.

Mkurugenzi wa Taasisi ya Chuo Kikuu cha Aga Khan ya Maendeleo ya Binadamu (IHD) Profesa. Kofi Marfo.

Hayo yamesemwa leo jijini Dar es Salaam na Naibu Katibu Mkuu wa Wizaya ya Elimu, Sayansi na Teknolojia Dk. Ave Maria Semakafu alipokuwa akifungua Mkutano wa Pili wa Kimataifa juu ya Maendeleo ya Watoto ulioandaliwa na Taasisi ya Chuo Kikuu cha Aga Khan ya Maendeleo ya Binadamu (IHD) kwa kushirikiana na Taasisi za The Conrad N. Hilton na Aga Khan.

Amesema pamoja na jitihada hizo za serikali, ametaka kuwepo kwa ushirikiano baina ya serikali na wadau mbalimbali wakiwemo Mashirika yasiyo ya kiserikali na jamii  katika kulinda watoto.
“Tunatakiwa kushirikiana na kusaidiana kwa pamoja katika kulinda haki za watoto,’’ amesema Semakafu.

Aidha ametaka mkutano huo uwe chachu ya kuja na mikakati ambayo itaboresha mazingira ya watoto katika maeneo ya elimu, afya, lishe, ukatili dhidi yao ili kuhakikisha changamoto zinazowakabili zinapatiwa ufumbuzi.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa taasisi ya IHD Profesa. Kofi Marfo, amesema kuwa kila mmoja anao wajibu kwa  maendeleo ya watoto ikiwa ni pamoja na  wazazi, familia, jamii na Taifa.

“Tuna jukumu la pamoja la kuhakikisha watoto wetu wanakua katika mazingira salama, kama vile wakati wa kucheza, maji salama ya kunywa, lishe bora, vituo vya afya na hospitali kwa ajili ya matibabu wakati wakiwa wagonjwa na mengine zaidi,” amesema Prof. Marfo.

Amewahimiza wadau  kutawa mkutano huo kutafuta mabadiliko ambayo yatafanya uwekezaji wa muda mrefu katika sera, huduma na mipango ambayo itaimarisha misingi ya Maendeleo ya Binadamu.

Naye Mkurugenzi wa Chuo Kikuu cha Aga Khan Profesa Joe Lugalla amesema mkutano huo utakuwa wa siku tatu unahusisha watifiti, wasomi na watunga sera na watajadili maendeleo ya watoto kwa kutatua changamoto zinazowakabili.


Mada zitakazo jadiliwa katika mkutano huo zitajumuisha utunzaji wa watoto wachanga, kushughulikia ukweli usio na wasiwasi, kuwawezesha wazazi  katika jamii za kipato cha chini namna ya kuhakikisha wanatunza watoto wao vizuri katika miaka miatatu ya kwanza ya maisha yao, kuboresha maendeleo ya watoto na afya ya akili ya uzazi.

Nyingine ni kusimamia tabia zisizofaa za wanafunzi wenye ulemavu wa utambuzi kabla ya usalama wa shule katika makazi yasiyo rasmi pamoja na masomo ya kesi inayotolewa katika Afrika, India, China na Paksitan.

  

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search