Polisi wakamata simu ya Zitto, kupekua ofisi ACT...soma habari kamili na Matukio360..#share

Na mwandishi wetu

JESHI la Polisi limeikamata simu ya kiongozi mkuu wa ACT Wazalendo, Zitto Kabwe na litapekua ofisi ya makau makuu ya chama hicho.

Zitto Kabwe

Katibu - Itikadi, Uenezi na Mawasiliano ya Umma wa ACT, Ado Shaibu  leo ameiambia Matukio360 kuwa Zitto aliripoti kituo cha Polisi Kamata jijini Dar es salaam kama alivyotakiwa awali na jeshi hilo.

‘Jeshi la Polisi limechukua simu ya ndugu Zitto kwa maelezo kuwa itasaidia uchunguzi wao, na wameahidi kuwa watairudisha kwake kesho jioni, na ametakiwa kurudi kituoni hapo Novemba 21, 2017,’ amesema Shaibu
  
‘Pia Jeshi la Polisi limetoa taarifa kuwa litakwenda katika Ofisi za Makao Makuu ya Chama cha ACT Wazalendo, kwa Lengo la kufanya upekuzi wa Ofisi hizo wakitafuta nyaraka zilizotumika na Chama kufanya Uchambuzi wa Takwimu za Serikali ambao unaonyesha Uchumi wa Nchi yetu "UNASINYAA".


About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search