Matibabu Harbinder Sethi utata! soma habari kamili na Matukio360..#share
Na
Abdulrahim Sadiki
HOSPITALI
ya Taifa ya Muhimbili(MNH) imedaiwa kushindwa kumfanyia Harbinder Sethi operesheni ya puto lililopo tumboni mwake. Hata hivyo Takukuru imepinga jambo hilo ikidai Muhimbili inauwezo wa kumtibu.
Harbinder Sethi wa kwanza kulia
Hayo
yamesemwa leo na wakili wa Sethi katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu na
kuiomba mahakama hiyo mteja wao atibiwe na daktari maalum kutoka nchini Afrika
Kusini.
Wakili
Joseph Sungwa amewasilisha ombi hilo leo mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu,Huduma
Shaidi mara baada ya mwendesha mashtaka wa Takukuru, Leonard Swai kudai kesi ilipangwa kutajwa na upelelezi wake bado
haujakamilika.
Baada
ya kutolewa kwa maelezo hayo, Wakili Sungwa aliwasilisha ombi hilo alieleza
kuwa anaomba Sethi kutibiwa na Daktari huyo maalum wa Afrika Kusini juu ya puto
ambalo linaisha muda wake kwa madai ya
kwamba Hospitali ya Taifa ya Muhimbili
hawawezi kufanya upasuaji huo.
Wakili
Sungwa amedai mteja wake baada ya
kufanyiwa vipimo Muhimbili, walimweleza hawawezi kufanya upasuaji wa puto.
Hivyo,
Wakili huyo aliomba daktari huyo wa Afrika Kusini aweze kuja kumtibia Sethi ama asafirishwe Afrika Kusini
kwa matibabu.
Swai
alipinga ombi hilo, akidai Muhimbili haijashindwa kumfanyia upasuaji wa puto Seth,
bali yeye mwenyewe ndiyo anajichelewesha kutokana na kutaka uwepo wa daktari
wake wa Afrika Kusini.
Alidai
kuwa mahakama hiyo ilikwishatoa amri
Sethi apelekwe Muhimbili kwa matibabu,
amri ambayo ilitekelezwa na hoja ya kwamba puto lililoko tumboni kwake limeisha
muda halijathibitishwa.
Alidai
ripoti ya daktari ni siri kati ya daktari na mgonjwa, hivyo hawezi kuisemea kwa
kuwa hawajaisoma lakini wanapata shaka la maelezo ya wakili wa Sethi kuwa
Muhimbili imeeleza kuwa haina
utaalamu wa kumfanyia upasuaji wa puto.
Swahi
amesema taarifa za Jeshi la Magereza ambako Sethi yupo na ripoti ya Hospitali ya Muhimbili
imepitia gereza alilopo na kwamba ni kweli hospitali hiyo ipo tayari na ina
uwezo wa kumfanyia upasuaji huo.
Mshtakiwa
alitueleza Magereza kuwa anahitaji daktari wake wa Afrika Kusini aje kumtibu,
lakini siyo kweli kwamba Tanzania hatuna uwezo wa kumtibu.
Alidai
kuwa suala hilo linahitaji utaratibu kwa
sababu linahusisha taasisi tofauti ambazo ni Magereza, Muhimbili na serikali.
Kuhusu
hoja ya Sethi kupelekwa Afrika Kusini,
Swai alidai ni ngumu na haiwezekani kabisa na hawaoni sababu ya kupelekwa huko
wakati Muhimbili wamethibitisha wanauwezo wa kumfanyia upasuaji wa puto.
Akielezea
upelelezi wa kesi hiyo, Swai alidai wapo katika hatua nzuri ambapo wanataka
kwenda mahabusu kuchukua maelezo ya onyo ya washtakiwa hao.
Swai
alidai amri ikitoka wachunguzi wataenda kuchukua maelezo yao.
Hoja
ya upelelezi iliibuliwa na Wakili Michael Ngalo, alidai upelelezi umechukua
muda mrefu ni takriban miezi mitano sasa haujakamilika na washitakiwa wapo
mahabusu.
Baada
ya kusikiliza hoja za mawakili wa pande zote husika, Hakimu Shaidi alisema juu
ya mshtakiwa ana uwezo wa kutibiwa Muhimbili ama la, mahakama hiyo haina
mamlaka ya kutoa amri yoyote hivyo wawasilishe maombi Mahakama Kuu.
Pia,
Hakimu Shaidi alikubaliana na ombi la wachunguzi kwenda kuchukua maelezo ya
onyo ya washitakiwa mahabusu. Hivyo siku ya Jumatatu watachukuliwa maelezo hayo
SAA 4 asubuhi.
Kesi hiyo iliahirishwa hadi Novemba 24, mwaka
huu.
Katika kesi hiyo, Sethi na James Rugemarila wanakabiliwa na mashtaka 12 ya
uhujumu uchumi kwa kula njama,
kujihusisha mtandao wa uhalifu , kighushi,
kutoa nyaraka za kughushi, kujipatia fedha kwa njia za udanganyifu, kutakatisha fedha na kuisababisha hasara ya USD 22, 198,544.60
na Sh 309,461,300,158.27.
No comments:
Post a Comment