Waziri mkuu awaonya askari polisi...soma habari kamili na Matukio360..#share

Na mwandishi wetu, Dodoma
SERIKALI imewaonya askari polisi kuacha vitendo vya kupigia raia kiholela na bila kuzingatia taratibu na maelekezo halali kutoka vyombo husika.


Waziri mkuu, Kassim Majaliwa akijibu maswali ya hapo kwa  hapo

Kauli hiyo imetolewa leo Bungeni Dodoma na Waziri mkuu Kassim Majaliwa alipokuwa akijibu maswali ya hapo kwa hapo kutoka kwa wabunge.

Akijibu swali kutoka kwa mbunge wa Kilwa, Modest Ng’ombare aliyetaka kujua kama serikali ipo tayari kuwalipa fidia baadhi ya masheikh kutokana na kupigwa na kujeruhiwa wakiwa  msikitini na askari polisi mwezi Julai, 2017.

"Mojawapo ya jukumu la jeshi la polisi ni kulinda raia na mali zao, sasa ikitokea watu wamejeruhiwa au kupigwa… jambo hilo linategemeana. Kama askari kafanya hivyo binafsi ni kosa na atachukuliwa hatua za kisheria. Na kama ni maagizo kutoka vyombo sahihi hilo linautaratibu wake wa jinsi ya kulishughulikia," alijibu waziri mkuu.

Akifafanua zaidi amesema askari polisi hatakiwa kumpiga raia na zaidi ni kumlinda na kuhakikisha usalama wake

Kuhusu muda wa kuwapo wafanyakazi wa kigeni nchini, waziri mkuu amesema sera inaelekeza wawepo kwa miaka miwili na kutoa utaalam(ujuzi) kwa watanzania.

"Hata hivyo sheria inaruhusu kumuongezea miaka miwili ikibainika kuwa watanzania bado hawajapata ipasavyo ujuzi kutoka kwa huyo mfanyakazi wa kigeni. Pia sheria hiyo inaelekeza mashirika na makampuni ya kigeni kuwa na kitengo maalum cha kutoa utaalam kwa watanzania." amesema

Kuhusu serikali kutenga fedha maalumu ya kununua taulo za wanafunzi wa kike, Waziri mkuu Majaliwa amesema serikali ipo katika mchakato wa kutatua tatizo hilo na kwamba kwa kuanzia tayari kila shule ina mwalimu wa kike anayehusika moja kwa moja na masuala ya ndani ya wanafunzi wa kike.

Kuhusu kukabilina na mabadiliko tabia nchi, waziri mkuu amesema serikali inakabiliana na suala hilo kupitia sheria ya mazingira inayoelekeza kutoa elimu kwa jamii  kuhifadhi mazingira popote walipo.





About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search