MCT yaonya uvunjifu wa haki za wanahabari...soma habari kamili na Matukio360..#share



Na Abraham Ntambara
BARAZA la Habari Tanzania (MCT) limesema takribani matukio 30 yameonyesha uvunjifu wa uhuru wa habari nchini.

Pia MCT  itawafikisha mahakamani  wote wanaowazuia, kuwanyanyasa na kuwapiga waandishi wa habari wawapo katika majukumu yao.


Katibu Mtendaji wa Baraza la Habari Tanzania (MCT) Kajubi Mukajanga  (Kulia) akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam.



Maelezo hayo yametolewa leo jijini Dar es Salaam na Katibu Mtendaji wa MCT, Kajubi Mukajanga katika maadhimisho ya siku ya Kimataifa ya Kupinga Jinai Dhidi ya Wanahabari, yanayofanyika duniani kote na kwamba baraza linachukua hatua hiyo kutokana na vitendo hivyo kushamiri .

“MCT haliridhishwi na mwenendo wa hali ya uhuru wa vyombo vya habari  nchini . Inasisitiza kuwa haki ya kupata habari na uhuru wa kujieleza ni haki ya  Kikatiba,” amesema Mukajanga.


Akitolea ukiikwaji wa haki hizo ni   katika kipindi cha miezi sita iliyopita magazeti matano yemefungiwa ambayo ni Mseto, Mwanahalisi, Mawio, Tanzania Daima na Raia Mwema.


Amesema mbali na kufungiwa kwa vyombo hivyo, waandishi mbali mbali wamepata misukosuko wakati wakiwa kazini. Baadhi yao ni Halfani Lihundi wa ITV Arusha, ambaye aliwekwa kizuizini na aliyekuwa Mkuu wa Wilaya ya Arumeru, Alexander Mnyeti.


Mwingine ni Augusta Njonji wa Nipashe ambaye hivi karibuni aliandika habari za Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC) na kukamatwa na kuhojiwa na polisi na baadae kuachiwa kwa dhamana.


Pia waandishi wa Mwananchi, Azam TV na Mtanzania huko Geita nao walipata msukosuko wakati wakiwa kazini kuripoti rabsha za wanafunzi wa Sekondari ya Geita hivi karibuni.


Matukio mengine amesema ni pamoja na waandishi Joel Maduka wa Storm FM na Vallence Robert wa Channel Ten kushambuliwa na polisi wakiwa kwenye msafara wa Waziri Mkuu mstaafu, Edward Lowassa huko Geita.


Wengine ni wapiga picha wa Kampuni ya The Guardian Ltd, Selean Mpochi na John Badi, ambao walinyang’anywa kamera zao wakati wakifanya kazi zao katika mkutano wa Sheikh Ponda katika hotel ya Iris ya jijini Dar es Salaam hivi karibuni.


Mukajanga amesema ukiukwaji mkubwa wa uhuru wa waandishi wa habari amekuwa ni kwa serikali kupitia polisi, wakuu wa mikoa na wilaya.


About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search