Ndovu afanyiwa upasuaji...soma habari kamili na Matukio360...#share

NDOVU mwenye uzito wa tani tano aliyepatikana kwenye shamba linalomilikiwa na walanguzi wa madawa ya kulevya, amefanyiwa upasuaji na hifadhi moja ya wanyama nchini Colombia.
Ndovu akifanyiwa upasuaji kwenye pembe yake
Ndovu huyo anayejulikana kwa jina la Tantor amefanyiwa upasuaji huo na watu takribani 30 kwa kudungwa dawa ya kumpa usingizi.
Kwa mujibu wa BBC ni kwamba upasuaji huo ulifanywa kwenye pembe yake iliyokuwa imepasuka.
Zaidi ya watu 100 walichanga pesa kwa upasuaji huo ambao uligharimu zaidi ya dola 8,500.
Upasuaji huo ungefanyika miaka miwila iliyopita wakati Tantor alijeruhi pembe yake, lakini shughuli hiyo ilichelewa baada ya kukosekana kwa vifaa vinavyostahili ili kufanya upasuaji.
Iibidi vifaa maalumu kutengenezwa kwa upasuaji huo.
Tantor alipekwa katika hifadhi ya Barranquilla Aprili mwaka 1991 wakati alipatwa na shirika la kupambana na madawa ya kulevya nchini Colombia kwenye shamba moja linalomilikiwa na walanguzi wa madawa ya kulevya.
Anaaminiwa kuwa na umri wa karibu miaka 50.


About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search