Miili 11 waliokufa ajali ya Ndege yapatikana...soma habari kamili na matukio

Na Mwandishi Wetu

MIILI ya watu 11 waliofariki katika ajali ya Ndege ya Shirika la Coastal Aviation iliyoanguka jana eneo Empakai Ngorongoro mkoani Arusha  imepatikana leo.


Ndege hiyo ilianguka baada ya kugonga mlima majira ya sasa saba mchana kutokana na matatizo ya hali ya hewa.

Mkuu wa Wilaya ya Karatu, Theresia Mahongo amesema zoezi la kutafuta miili limekwenda vizuri.

"Miili yote imepatikana na tutaipeleka Karatu na baadaye Arusha," amesema.

Naibu Mhifadhi wa hifadhi ya Ngorongoro, Dk Maurus Msuha amesema wamefanikiwa kuipata miili na kuitoa eneo la ajali kutokana na ushirikiano mkubwa na wenyeji.

"Tuliwaomba kulala hapa wenyeji jana kuilinda isiliwe na wanyama na hadi leo tumeikuta miili salama," amesema.


Mmoja wa mashuhuda wa ajali hiyo, Lunda Mollel amesema ndege hiyo kabla ya kuanguka ilikuwa inazunguka kutoka eneo la milima zaidi ya dakika 20 hadi baadaye kuanguka baada ya kugonga mlima.

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search