Operesheni kamata 'bodaboda' yaanza...soma habari kamili na Matukio360..#share

 Na Salha Mohamed

JESHI la Polisi kikosi cha Usalama barabarani, limeanza operesheni ya kukamata madereva pikipiki wanaovunja sheria .


MKUU wa kikosi cha Usalama wa Polisi barabarani, Kanda Maalum ya Dar es Salaam,  Marisone Mwakyoma (katikati) akizungumza na waandishi wa habari juu ya  maadhimisho ya wiki ya nenda kwa usalama katika Kanda hiyo yanayotarajia kufunguliwa na Mkuu wa Mkoa huo, Paul Makonda Novemba 18/2017 katika viwanja vya biafra.

Agizo hilo limetangazwa leo jijini Dar es Salaam  na Mkuu wa kikosi cha Usalama barabarani Kanda ya Dar es Salaam, SSP Marisone Mwakyoma alipokuwa akizungumzia maandalizi ya maadhimisho ya wiki ya nenda kwa usalama yanayotarajia kuanza Novemba 18-23/2017.

"Tumeshaunda kikosi kazi kwa Kanda ya Dar es Salaam, tumeanza operesheni, kwa dereva atakayekiuka sheria makusudi tutamchukulia hatua  kwake na kwa jamii nzima, "amesema.

Amesema operesheni wanazofanya hadi sasa zimepunguza ajali kwa asilimia 25.

Mwakyoma amefafanua kuwa wana kamera za kisasa zinazopiga picha madereva watakaovunja sheria na kuwakimbia polisi hata nje ya eneo la tukio.

"Hatuhitaji kuwakimbiza, tutawakamata huko huko, "amesema  kuongeza kuwa madereva wanapaswa kusomea ili kujua mabadiliko ya sheria za barabarani.

Amesema dereva anapokamatwa na trafiki kwanza anapaswa kujua kosa lake na kukubaliana nalo au kujitetea kabla ya kuandikiwa kulipa faini.

" Hatuhitaji trafiki anayemwandikia mtu kosa moja kwa moja, anapaswa kumwambia kosa gani amefanya, aridhike amwandikie au waende mahakamani, "amesema.

Amesema jijini Dar es Salaam  makosa yanayoongoza kufanywa ni kupakia mizigo kwenye gari la abiria, kukatisha njia na  kupita pembezoni mwa barabara.

Mengine ni ulevi, kutovaa sare, kutokuwa na tiketi na kuendesha kwa mwendo hatarishi.

Maadhimisho hayo yanatarajia kufunguliwa na Mkuu wa mkoa huo, Paul Makonda katika viwanja vya Biafra yenye Kauli mbiu 'Zuia ajali, Tii Sheria - Okoa maisha'



About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search