Wizara ya Maji, Tanesco kuvunjwa...soma habari kamili na Matukio360..#share

Na mwandishi wetu
RAIS Dk John Magufuli ameagiza jengo  la makao makuu ya shirika la umeme(Tanesco) na lile la wizara ya maji lililopo Ubungo kuwekewa alama ya X ili kuvunjwa.

Makao Makuu ya Tanesco

Ametoa agizo hilo leo jijini Dar es Salaam alipokuwa katika ziara ya kukagua ujenzi wa daraja la ghorofa tatu  makutano ya barabara eneo la Ubungo

"Ikiwezekana leo au kesho muweke x katika jengo la Tanesco na lile la wizara ya maji ambapo ukuta wake upo sehemu ya ndani ya barabara. Sheria ni msumeno hata serikali ikifanya kosa inasurubiwa na hata raia akijenga kwenye hifadhi ya barabara anasurubiwa," amesema rais na kuongeza

"Sheria ya hifadhi ya barabara ilianza tangu mwaka 1932 ikafanyiwa mabadiliko mwaka 1959,1963 na 1997 ukubwa wa barabara Morogoro kutoka mjini ni mita 22.5 kwa 22.5."


About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search