Mugabe ateta na mkuu majeshi Zimbabwe...soma habari kamili na Matukio360..#share
Na
mashirika ya kimataifa
WAKATI
Jeshi nchini Zimbabwe linamzuilia rais Robert Mugabe nyumbani kwake katika mji
mkuu wa nchi hiyo Harare amezungumza na mkuu wa majeshi wa nchi hiyo, Jen
Constantino Chiwenga
Mkutano kati ya rais Robert Mugabe na mkuu wa majeshi ya Zimbabwe Jen Constantino Chiwenga pamoja na wajumbe kutoka Afrika Kusini katika ikulu ya rais Harare zimetolewa.
Mugabe
ambaye hana mpango wa kujiuzulu kwa hiari alimwambia rais wa Afrika Kusini
Jocub Zuma kwa njia ya simu kwamba yuko salama.
Hatua
za kijeshi zilifuatia baada ya kufutwa
kwa Makamu wa Rais Emmerson Mnangagwa ambaye ni hasimu mkubwa wa wa mke wa Mugabe, Bi Grace Mugabe.
Hata
hivyo kiongozi wa upinzani nchini humo Morgan Tsvangirai amemtaka Mugabe
ajiuzulu wa hiari kabla ya uchaguzi unaotarajiwa kufanyika mwakani.
Wanajeshi
wanashika doria katika barabara za Harare baada ya kuchukua udhibiti wa runinga
ya taifa katika kile walichosema ni juhudi za kuwaandama "wahalifu".
Hatua
hiyo huenda ikawa juhudi za kutaka kumuondoa madarakani Mugabe na badala yake
kumuingiza madarakani makamu wake wa rais Emmerson Mnangagwa, ambaye alimfuta
kazi wiki iliyopita.
Kufutwa
kwa Mnangagwa wiki iliyopita kulikuwa
kumemuweka mke wa Rais Mugabe, Grace, katika nafasi nzuri ya kumrithi.
Mugabe, 93, ameongoza taifa hilo tangu
lilipojipatia uhuru mwaka 1980 kutoka kwa Uingereza.
Wanajeshi
nchini Zimbabwe walichukua udhibiti wa kituo cha taifa cha utangazaji usiku na
milipuko mikubwa ilisikika pamoja na ufyatuaji wa risasi usiku kucha mjini
Harare.
Jenerali
mmoja wa jeshi alitokea kwenye runinga na kusisitiza kwamba hakujatekelezwa
mapinduzi ya kijeshi.
Alisema
Rais Robert Mugabe na familia yake "wako salama salimini."
Lakini
mzozo kuhusu ni nani anaweza kumrithi Mugabe kati ya Bi Grace Mugabe na Bwa
Mnangagwa umekigawanya chama cha Zanu-PF miezi ya hivi karibuni.
Nchi
za Jumuia ya maendeo ya kusini mwa Afrika (SADC) jana (Alhamisi) zilifanya mkutano wa dharura nchini Botswana.
Umoja
wa Afrika (AU) umesema hatua ya jeshi la
Zimbabwe ni kama mapinduzi
Siku
ya Jumatano wanajeshi wakiwa na magari ya jeshi walilizinga bunge na majengo
mengine makuu ya serikali.
Saa
kadha baadaye walichukua udhibiti wa makao ya kituo cha habari cha serikali ZBC
na kutangaza kuwa walikuwa wanawalenga waalifu wanamzunguka Rais Mugabe.
Hata
hivyo meja Jenerali Sibusiso Moyo alikana kuwa hakukukuwa na mapinduzi wa kijeshi
na kuwa Mugabe na familia yake walikuwa salama.
No comments:
Post a Comment