Mwanasheria ataka wanasiasa 'uchwara' wapuuzwe...soma habari kamili na Matukio360..#share
Na
Salha Mohamed
WANANCHI
wametakiwa kuwapuuza wanasiasa wanaopinga miradi ya serikali na kwamba wanajali
maslahi binafsi na si hamaendeleo ya taifa.
Wakili wa kujitegemea, Leonard Manyama
akizungumza na waandishi wa
habari(hawapo pichani) kutoa tamko la kuunga mkono uongozi wa rais John
Magufuli katika kipindi cha miaka miwili
Wito
huo umetolewa leo jijini Dar es Salaam na wakili wa kujitegemea, Leonard
Manyama wakati akitoa tamko la kuunga mkono uongozi wa miaka miwili wa rais
John Magufuli
"Tuwapuuze
wanasiasa wanaopinga miradi mikubwa ya maendeleo inayotekelezwa na serikali
kama ujenzi wa treni ya kisasa, mradi wa umeme wa Stiglas na ununuzi wa ndege,
"amesema.
Amesema
miradi hiyo ina manufaa kwa taifa na
kuiunga mkono serikali hata kama inakopa fedha za miradi hiyo.
"
Tuwapuuze wanasiasa wanaotuaminisha kuwa serikali hii ni mbovu eti hakuna fedha
mifukoni, fedha zitapatikana kwa kufanya kazi kwa bidii na si kwa madili
haramu, "amesema.
Manyama
amesema wapo baadhi ya wanasiasa
wanaokwepa kulipa kodi huku wengine walikuwa serikalini na kutumia nafasi zao
kujilimbikizia mali, mashamba na kujibinafsisha au kuuza Viwanda.
"
Hawa ni watu hatari sana si wa kuwaunga mkono hata kidogo wanapaswa kuolewa a
kupuuzwa.. .. Hadi 2020 tutawajua wanasiasa wazalendo na wanasiasa matapeli na
wenye nia binafsi, "amesema.
Amesema
rais Magufuli amekuwa akipambana na rushwa, ufisadi, kudhibiti ukwepaji wa
kulipa kodi, kuimarisha kwa vita dhidi ya biashara haramu ya dawa za kulevya,
ujangili na mapambano dhidi ya rasilimali kama madini.
No comments:
Post a Comment