NEC kutangaza uchaguzi majimbo mawili, kata tano zilizo wazi...soma habari kamili na Matukio360..#share
Na mwandishi wetu
TUME ya taifa ya uchaguzi(Nec) imepokea taarifa rasmi ya kuwapo kwa majimbo mawili na kata tano zilizowazi kufuatia wabunge na madiwani kujiuzulu na wengine uteuzi wao kutenguliwa na mahakama.
TUME ya taifa ya uchaguzi(Nec) imepokea taarifa rasmi ya kuwapo kwa majimbo mawili na kata tano zilizowazi kufuatia wabunge na madiwani kujiuzulu na wengine uteuzi wao kutenguliwa na mahakama.
Watendaji wa kuu wa NEC wakipitia baadhi ya nyaraka kuhusu uchaguzi
Kufuatia hali hiyo NEC inatarajia kutangaza marudio ya uchaguzi mdogo katika majimbo na kata hizo
Soma taarifa kamili
Tume ya Taifa ya
Uchaguzi imepokea taarifa kutoka kwa Mhe. Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano
wa Tanzania akiitaarifu kuwepo kwa nafasi wazi ya Ubunge katika Jimbo la
Singida Kaskazini kufuatia Ndugu Lazaro Samwel Nyalandu kuvuliwa Uanachama wa Chama
cha Mapinduzi (CCM) na hivyo kupoteza sifa ya kuwa Mbunge.
Aidha, kwa mujibu
kifungu cha 113(1) cha Sheria ya Taifa ya Uchaguzi, Sura ya 343, Tume imepokea
Hati ya Mahakama Kuu ya Tanzania ikithibitisha uamuzi wa Mahakama hiyo juu ya kutengua
matokeo ya Uchaguzi wa Mbunge wa Jimbo la Longido ambalo Ndugu Onesmo Ole
Nangole alikuwa ni Mbunge.
Wakati huo huo
Waziri mwenye dhamana ya Serikali za Mitaa kwa kutumia mamlaka aliyopewa chini
ya kifungu cha 13(1) cha Sheria ya Uchaguzi ya Serikali za Mitaa, ameitaarifu
Tume uwepo wa nafasi wazi za Madiwani katika Kata tano zilizopo katika
Halmashauri mbalimbali.
Kwa kuzingatia
masharti ya Sheria ya Taifa ya Uchaguzi Sheria ya Uchaguzi ya Serikali za
Mitaa, Tume ya Taifa ya Uchaguzi itatoa ratiba ya Uchaguzi Mdogo wa kujaza
nafasi wazi za Majimbo na Kata hizo hapo baadae.
Majimbo na Kata
zilizo wazi ni kama ifuatavyo:-
Jedwali Na. 1:
Majimbo yaliyowazi
NA.
|
MKOA
|
HALMASHAURI
|
JIMBO
|
1.
|
Singida
|
Halmashauri
ya Wilaya ya Singida
|
Singida
Kaskazini
|
2.
|
Arusha
|
Halmashauri
ya Wilaya ya Longido
|
Longido
|
Jedwali Na. 2: Kata zilizowazi
NA.
|
MKOA
|
NA.
|
HALMASHAURI
|
NA.
|
KATA
|
1.
|
Kagera
|
1.
|
Halmashauri ya Wilaya ya Ngara.
|
1
|
Keza
|
2.
|
Arusha
|
2
|
Halmashauri ya Jiji la Arusha
|
2
|
Kimandolu
|
3.
|
Pwani
|
3.
|
Halmashauri ya Wilaya ya
Kisarawe.
|
3
|
Kurui
|
4.
|
Tabora
|
4.
|
Halmashauri ya Wilaya ya
Tabora
|
4
|
Bukumbi
|
5.
|
Tanga
|
5.
|
Halmashauri ya Wilaya ya
Korogwe.
|
5
|
Kwagunda
|
Jaji (R)
Semistocles S. Kaijage
MWENYEKITI
TUME YA TAIFA YA UCHAGUZI
16 NOVEMBA, 2017
No comments:
Post a Comment